LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Mar 30, 2026

KANISA HALISI HALIPOI, KUUNGURUMISHA MKUTANO MKUU JUMAPILI IJAYO, LANGO LA 12 TAMUZI 1MH, KAO KUU, JIJINI DAR ES SALAAM

Na Bashir Nkoromo, Tegeta.
Maelfu ya Uzao Halisi na Watekeleza Sauti Halisi wa Kanisa Halisi la Muumba kutoka Mataifa mbalimbali, ndani na nje ya Tanzania wanatarajiwa kuhudhuria Mkutano Mkuu wa Kanisa hilo, utakaorindima, Lango la  12 Tamuzi 1 Majira Halisi (Jumapili, Aprili 5, 2026), Kao Kuu, Tegeta Namanga, Plot. 195, Jijini Dar es Salaam.

Baba Halisi amesema, mbali na Watekeleza Sauti Halisi na Uzao Halisi kutoka mataifa mbalimbali ndani na nje ya Tanzania viongozi na wageni mbalimbali wamealikwa kuhudhuria mkutano huo bila kubagua, kwa kuwa Kanisa Halisi ni la wote.

Amesema, pamoja na mambo mengine, Mkutano huo utafanya maboresho mengi makubwa ikiwemo ya safu za uongozi katika ngazi mbalimbali ambapo baadhi ya nafasi ambazo hazikuwepo zitaongezwa.

Baba Halisi amesema, Mkutano huo utafanyika Sanjari na Ibada maalum, itakayotangulia, na amewakaribisha kwa upendo Uzao Halisi na Watekeleza Sauti kuhakikisha kila mmoja hakosi kuhudhuria kwenye Ibada na mkutano huo kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 8 mchana.


No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages