LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Feb 16, 2026

SIMU JANJA KUTUMIKA KUENDESHA MAFUNZO VETA

ILI kuwapa vijana na wananchi wengine uhuru zaidi wa kujifunza mafunzo ya, ufundi stadi popote walipo na kwa muda wao, Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeanzisha mfumo uitwao VSOMO unaomwezesha mwanafunzi kujifunza maarifa yote ya ufundi stadi kwa kutumia simu ya mkononi, kufanya mtihani kwenye simu hadi mwisho wa mpango wa mafunzo ya nadharia.

Mfumo huo umeelezwa na Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Anthony Kasore alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari kwenye Ukumbi wa Wizara ya Habari,Utamaduni Sanaa na Michezo katika Mji Serikali Mtumba jijini Dodoma Februari16, 2026, kuhusu mafanikio ya utekelezaji wa siku 100 wa ahadi zilizotolewa na Rais Samia alipoapishwa Novemba 3, 2025.

Baada ya hapo, atapangiwa kufanya mafunzo ya vitendo kwenye chuo kimojawapo cha VETA. Hii inapunguza muda wa kukaa chuoni na inaongeza matumizi bora ya simu za mkononi na muda wa mafunzo. Vilevile, mpango huu unawapa fursa watu walio mbali na vyuo kupata mafunzo ya ufundi stadi,”amesema  CPA Masore.

“VSOMO ilikuwa ikitekelezwa kwa ushirikiano wa VETA, Airtel na Kampuni ya Magilla Tech. Hata hivyo, mwaka jana, VETA ilikabidhiwa rasmi mfumo huu ambapo kwa sasa VSOMO inapatikana kupitia mitandao yote ya simu iliyopo nchini. “

Ametaja stadi zipatazo ishirini (20) zinazotolewa kupitia mfumo wa VSOMO, kuwa ni; Ufundi wa Pikipiki; Ufundi wa Umeme;  Ufundi wa Aluminium na PVC; Umeme wa Magari; Utandazaji na Ufungaji Mabomba; Utengenezaji wa Kompyuta; Upishi na Utoaji Huduma ya Chakula (Catering); Uokaji Mikate na Upambaji; Usafi wa Majengo Makubwa na Maeneo ya Umma; Maua na Upambaji kwenye Shughuli; Ujasiriamali; Utengenezaji wa Simu za Mkononi; Ufungaji Mabomba Viwandani; Umeme wa Viwandani; Uungaji Vyuma Viwandani na Urembo.

Mpaka sasa Takribani wanafunzi 533 wamemaliza kozi mbalimbali kupitia mfumo huu wa VSOMO na kutunikiwa vyeti.

Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Antony Masore.
Wanahabari wakisikiliza kwa makini katika mkutano huo.

Baadhi ya viongozi wa Idara ya Habari MAELEZO na VETA wakiwa katika mkutano huo.


Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO, Kelvin Kanje akihitimisha mkutano huo.

IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA - 0754264203

No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages