Waziri wa Afya Jenista Mhagama akimkabidhi tuzo Alhaj Dk Mzimbiri ambaye aliibuka mshindi wa tuzo za Tafiti za Kansa. hafla hiyo ilifanyika Hospitali ya Shifaa iliyopo jijini Dar es Salaam, hivi karibuni.
Alhaj Dk. Mzimbiri ambaye amesomea taaluma yake nchini China, India na Marekani mbali na tafiti za kansa amekuwa akitia elimu kuhusu ugonjwa huo kwa kuendesha vipindi vya afya katika vyombo vya Habari vya kitaifa na kimataifa kama Azam Tv, BBC na televisheni ya Umoja wa Mataifa (UN Tv).

No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇