Jun 5, 2025

MIKAKATI YA MSAJILI WA HAZINA KUIMARISHA MASHIRIKA KUENDANA PIA NA ILANI YA CCM YA 2025/30

Na Bashir Nkoromo, CCM's Blog
Msajili wa Hazina Nehemiah Mchechu amesema, Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) katika mikakati yake ya kuendelea kuboresha taasisi na mashirika ya umma kuwa imara kiuchumi itachukua pia baadhi ya maelekezo kutoka kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya 2025/30.

"Katika mikakati yetu ya kuimarisha mashirika na tasisi za umma kuna baadhi ya mambo tutaçhukua kutoka katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM ili kurandana na maelekezo ya Chama kilichounda serikali", alisema Mchechu kujibu swali la mwandishi wa habari hii, aliyetaka kujua kama anaionaje Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2025/30 iliyozinduliwa  wakati wa Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Mei Mei 30 mjini Dodoma.

Mwandishi wetu alipata fursa ya kuuliza swali hilo, baada ya Mchechu kumaliza Kikao kazi na Wahariri wa Habari kilichofanyika Jumatatu, Juni 2, 2025 katika Hotel ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam, ambapo aliwasilisha kwa hawariri hao taarifa  kuhusu safari ya Mageuzi, Mafanikio, Mikakati  na Muelekeo  wa taasisi na mashirika y umma nchini. 

Msajili wa Hazina Nehemiah Mchechu akizungumza katika kikaokazi chake na Wahariri wa habari kilichofanyika Jumatatu, Juni 2, 2025 katika Hotel ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam, kuwasilisha taarifa  kuhusu safari ya mageuzi, mafanikio, mikakati  na uelekeo  wa taasisi na mashirika ya umma nchini. Tafadhali soma wasilisho hilo kama aliyolitoa.👇

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Pages