LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 12, 2024

MAPOKEZI YA RAIS SAMIA MWANZA

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewasili mkoani Mwanza kwa ajili ya ziara maalum ya kikazi na kupokelewa na viongozi wa Chama na Serikali, wakiongozwa na Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Ndugu Juma Mtanda, leo mchana tarehe 12 Oktoba 2024. Akiwa njiani kutoka Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Mwanza, Mhe. Dkt. Samia alipata fursa ya kuzungumza na wananchi katika eneo la Pasiansi, jijini Mwanza

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM, Dk. Samia akilakiwa na Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Nchimbi, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza Michael Lushinge pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda.

Rais Samia akizungumza na wananchi.
Sehemu ya umati wa watu waliofika kumlaki Rais Samia.



Rais Samia akilakiwa na baadhi ya viongozi alipowasili Uwanja wa Ndege wa Mwanza.


 

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages