LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 20, 2024

CHATANDA APITA MTAA KWA MTAA TANGA MJINI KUHAMASISHA WANANCHI KWENDA KUJIANDIKISHA

 Na Mwandishi Wetu, Tanga Mjini

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania (UWT), Ndg. Mary Pius Chatanda (MCC) amewataka wanawake wote nchini kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali bila kuogopa lolote lile.

Aidha, Chatanda amewataka wanaume wote kuendelea kuwaunga mkono wanawake wenye karama na uwezo mkubwa wa uongozi na bila ubaguzi wowote ule.

Aidha, amehimiza wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la wapiga kura kwa ajili ya kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Novemba 27, 2024. Uandikishaji untamatika leo.

Ameyasme hayo alipotinga mitaani mjini Tanga kuhamasissha wananchi kwenda kujiandikisha katika daftari hilo.

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania (UWT), Ndg. Mary Pius Chatanda akiwahamasisha wanawake kwenda kujiandikisha alipokuwa akipita katika mitaa mbalimbali jijini Tanga.

Chatanda akizungumza na mmoja wa akina mama kwa lengo la kumhamasissha kwenda kujiandikisha. Nyuma yake ni Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini, Ummy Mwalimu.

Chatanda akiwa na baadhi ya viongozi wakipita mtaa kwa mtaa kuhamasisha wananchi kwenda kujiandikisha.
Chatanda akizungumza na baadhi ya wanawake wakati wa tukio hilo la luwahamasisha wananchi kwenda kujiandikisha.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages