NA VICTOR MAKINDA.
Chama Cha Mapinduzi (CCM), wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro, kimetoa wito kwa watu wanaoishi na ulemavu wenye sifa za kugombea uongozi, kujitokeza kuwania nafasi mbali mbali katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kilombero, Mohamed Msuya, mjini Ifakara leo.
Msuya amesema kuwa CCM ni chama cha watu wote na chama hicho hakimbagui yeyote hivyo kinatoa witu kwa watu wanaoishi na elemavu na wanawake wenye sifa za kugombea kujitokeza kwa wingi.
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇