LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Aug 7, 2024

ZAIBUKA SHANGWE BAADA YA DK NCHIMBI KUMWAGIZA WAZIRI AWESO KWENDA KUTATUA KERO YA MAJI KAMUNAZI NGARA

 


 Wananchi  Kijiji cha Kamunazi wilayani Ngara, Kagera, wakiwa na furaha kumsikia  Waziri wa Maji, Jumaa Aweso akijibu kupitia simu aliyompigia Katibu Mkuu wa CCM, Dk Emmanuel Nchimbi akimuagiza aende kijijini hapo kutatua kero ya maji. 


DK. Nchimbi ametoa utatuzi huo msafara wake uliposimamishwa na wananchi wa eneo hilo na kutoa kero ya maji na umeme smba umefika kwa kuwasha transfoma lakini bila kuwaunganishia wananchi.

Msafara wake ulikuwa unatoka Biharamulo kwenda Ngara kuwahi kuhutubia mkutano wa hadhara.

DK Nchimbi ameanza jana ziara ya kikazi mkoani Kagera, baada ya kumaliza katika Mkoa wa Kigoma.

No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages