LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Aug 7, 2024

DK NCHIMBI KUFANYA MKUTANO MKUBWA NGARA


 


 Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi DK. Emmanuel Nchimbi na msafara wake kutinga Wilaya Ngara mkoani Kagera utakakofanyika mkutano mkubwa wa hadhara.


Asubuhi hii kabla ya kwenda Ngara atafanya mkutano wa ndani na viongozi mbalimbali wa CCM wa wilaya ya Biharamulo.


DK Nchimbi Jana alihitimisha ziara yake mkoani Kigoma kwa kuwasalimia wananchi Wilaya ya Kibondo, Kakonko na hatimaye kuingia Mkoa wa Kagera kwa kuwasalimia wananchi eneo la Nyakanazi wilayani Biharamulo.


Baada ya Dk Nchimbi kumaliza ziara Kagera  ataendelea na ziara katika mikoa mingine  ya Kanda ya Ziwa ambayo ni;  Geita, Mara na Mwanza.


Malengo ya ziara hiyo ni; Kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020, kuhuisha uhai wa chama, kusikiliza na kutatua kero za wananchi pamoja na kuhamasisha wananchi kujitokeza kuhakiki taarifa zao na kujiandikisha katika Kitabu cha Kudumu cha Wapiga kura, kwa ajili ya maandalizi ya Uchaguzi wa serikali za mitaa Novemba mwaka huu.

Balozi Dk. Nchimbi, kwenye hiyo ameambatana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) - Oganaizesheni, Issa Haji Usi Gavu, Katibu wa NEC - Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla Katibu wa NEC - Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Rabia Hamid Abdallah,

No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages