LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 23, 2024

ZIARA YA MBUNGE NJEZA YAZIDI KURINDIMA MBEYA VIJIJINI


Mbunge wa Mbeya Vijijini, Oran Njeza akiwa katika matukio mbalimbali wakati wa ziara yake ya kikazi jimboni kwake Julai 22, 2024.





Mbunge wa Mbeya Vijijini, Oran Njeza anaendelea na ziara yake katika kata mbalimbali jimboni humo kwa kutoa michango mbalimbali pamoja na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo.

 

Mbunge huyo katika ziara yake ya jana ametoa sh. 400,000 kwa ajili ya kusaidia chakula cha wanafunzi wawapo shuleni, ambapo sh. 200,000 imepewa Shule ya Msingi Chang'ombe na sh. 200,000 nyingine ameipatia Shule ya Msingi Itega.

 

Hata hivyo, amewaomba wananchi nao kuendelea kuwa na moyo wa kujitolea katika ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo jimboni humo, bila kusahau kutoa michango kwa ajili ya chakula cha wanafunzi shuleni.

 

Aidha, akiwa katika Kijiji cha Chang’ombe alitatua changamoto ya muda mrefu ya maji kiasi cha kupata pongezi kutoka kwa wananchi kwa kuwajali.

 

Mbunge huyo ametoa ahadi kuanzia mwaka huu, kutoa zawadi ya sh. 100,000 kwa kila mwanafunzi wa darasa la saba jimboni humo atakayepata ufaulu wa daraja A kwa lengo la kuhamasisha ufaulu.

 

Njeza ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, amewaeleza wananchi wa Kata ya Mjele, kwamba  serikali imetenga sh. milioni 50 kwa ajili ya ukarabati wa Shule ya Msingi Itega, jambo ambalo lilipokelewa kwa furaha kubwa na wananchi wa eneo hilo. 

 

 Pamoja na mambo mengine, lengo la ziara hiyo ni; kukagua miradi ya maendeleo ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi 2020, kusikiliza na kutatua kero za wananchi pamoja na kuhuisha uhai wa chama pamoja na kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kuhakiki taarifa zao kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, zoezi litakapoanza jimboni humo.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages