LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 26, 2024

POLISI Z'BAR YAMNYAKA KWA KUJIZOLEA SH. MILIONI 6, AKITAPELI KUSETI AJIRA USALAMA WA TAIFA NA KIKOSI CHA SERIKALI YA MAPINDUZI

Polisi, Zanzibar
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi linamshikilia Marco Daud Zagamba (32) wa Mbweni, kwa tuhuma za kujipatia sh. milioni 6 kwa njia ya utapele wa kuwapatia ajira watu mbalimbali kati Idara ya Usalama wa Taifa na vikosi vya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Madema, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi ACP Abubakar Khamis Ally amesema mtuhumiwa huyo aliwatapeli wananchi kwa kuwaahidi kuwapatia ajira kwenye Vikosi vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Idara ya Usalama wa Taifa.

Amefafanua kwamba mtuhumiwa huyo hutumia mbinu ya kujifanya mtumishi wa Serikali na kuwa ana uwezo wa kutoa ajira ambapo alifanya hivyo akijua kuwa ni kinyume cha sheria.

Ametoa mwito kwa wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya watuhumiwa wa utapeli hasa kipindi hiki ambacho Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP. Camillus Wambura ametangaza usaili kwa waombaji wa ajira za Jeshi la Polisi.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi ACP Abubakar Khamis Ally akizungumza na Waandishi wa Habari, Ofisini kwake Madema, Zanzibara, jana, 

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages