LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 21, 2024

NAIBU WAZIRI BALOZI KASSIM MBAROUK AJIUZULU UBUNGE, LEO

Ofisi ya Bunge, Dodoma
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk amejiuzulu Ubunge wa kuteuliwa na Rais.

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Bunge, imesema  Mbarouk amejiuzulu kwa kumuandikia Spika wa Bunge Dk. Tulia Ackson leo Jumapili Julai 21, 2024.
 
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Mbarouk amesema amefikia  uamuzi huo kufuatia changamoto za kijamii zinazomkabili kwa sasa.

“Ninalazimika kuchukua uamuzi wa kujiuzulu ili nipate nafasi ya kushughulikia changamoto hizo,” amesema Mbarouk katika barua yake ya kujiuzulu Ubunge.

Balozi Mbarouk pia amewahi kuhudumu katika Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI).

Balozi Mbarouk

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages