LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 30, 2024

MAPOKEZI YA DK NCHIMBI MKOA WA LINDI

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), DK Emmanuel Nchimbi akivishwa skafu  wakati wa mapokezi rasmi alipowasili kuhudhuria kikao cha Kamati ya Siasa katika Ofisi za Mkoa wa Lindi asubuhi hii tayari kuanza rasmi ziara mkoani humo. 

Baada ya hapo atafanya mkutano wa ndani wa viongozi wa chama wa Mkoa huo.

Lengo la ziara hiyo ni; Kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020, kuhuisha uhai wa chama, kusikiliza na kutatua kero za wananchi pamoja na kuhamasisha wananchi kujitokeza kuhakiki Taarifa zao na kujiandikisha katika kitabu Cha kudumu Cha Wapiga kura, kwa ajili ya maandalizi ya Uchaguzi wa serikali za mitaa Novemba mwaka huu.


Katika ziara hii, Dk. Nchimbi  ameambatana na Katibu wa NEC-Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndg. Amosi Makalla, Katibu wa NEC-Organaizesheni Ndg. Issa Ussi Haji (Gavu) pamoja na Katibu wa NEC- Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndg. Rabia Abdallah Hamid.




Dk Nchimbi akisalimiana na viongozi mbalimbali.

Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Amos Makalla akisalimiana na viongozi mbalimbali.


IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA

0754264203
 

No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages