Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Balozi Ndg. Dkt. Emmanuel Nchimbi leo Julai 28 amepokelewa na Wanachama pamoja na Wananchi wa Mkoa wa Mtwara katika Uwanja wa Ndege wa Masasi tayari kwa kuanza Ziara yake ya Mikoa Miwili ya Kusini Mtwara na Lindi .
Katika ziara hii Dk Nchimbi ameambatana na Katibu wa NEC-Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndg. Amosi Makalla, Katibu wa NEC-Organaizesheni Ndg. Issa Ussi Haji (Gavu) pamoja na Katibu wa NEC- Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndg. Rabia Abdallah Hamid.
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇