Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akisisitiza watanzania bila kujali itikadi zao kuilinda amani ya nchi alipokuwa akihutubia katika mkutano wa ndani wakati wa ziara yake mkoani Katavi Aprili mwaka huu.
Katika ziara yake ya kikazi ya siku 10 katika mikoa 6 ya Katavi, Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Ruvuma, Dkt Nchimbi alihamasisha uhai wa chama, kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi, kuelezea maandalizi ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025 pamoja na kukagua utekelezaji wa Ilani ya chama.
Wakati wa ziara hiyo Dkt Nchimbi aliambatana na wajumbe wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM, Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla na Katibu wa Oganaizesheni, Issa Haji Gavu. Iilianzia Katavi Aprili 13 na kumalizia Ruvuma Aprili 23, 2024.
MHARIRI
BLOG YA TAIFA YA CCM
0754264203
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇