Baada ya kusikiliza kero za wananchi wa eneo hilo aliwashukuru kwa mapokezi mazuri yaliyoambatana na ngoma mbalimbali za asili, alisikiliza kero za wananchi na baadhi kuzitafutia ufumbuzi kwa kuwaita viongozi wa Taasisi kujibu majibu sahihi na jinsi ya kuzitatua.
Kero zilizowasilishwa ni uhaba wa maji, miundombinu ya barabara na ujenzi wa Kituo cha Afya eneo hilo ambacho aliahidi kuweka msukumo wa kipekee kuhakikisha kinajengwa haraka kunusuru vifo vya wagonjwa wanaosafirishwa umbali mrefu kwenda kupata matibabu katika vituo ama hospitali za mbali..
Katika ziara hiyo, Dk Nchimbi ameambatana na Wajumbe wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM, Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla, Katibu wa Oganaizesheni, Issa Haji Gavu na Katibu wa Idara ya Uchumi na Fedha, Dk Frank Hawasi.
Lengo la ziara hiyo ya siku 10 katika mikoa 6 ni kuimarisha uhai wa chama kuanzia ngazi ya mashina, kusikiliza kero na kuzitafutia ufumbuzi, kuelezea maandalizi ya uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu mwakani, kukagua miradi ya maendeleo ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya CCM
Dk Nchimbi akiangalia na kufurahishwa na ngoma mbalimbali za asili ikiwemo mganda, chihoda
Akitia saini katika kitabu cha kumbukumbu
Mbunge wa Jimbo la Nyasa, Stelah Manyanya akielezea mambo mengi ya maendeleo yaliyonywa wakati wa kipindi chake cha uongozi katika jimbo hilo.
Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Dk Nchimbi kuanza kuzungumza na wananchi.
Katibu wa Oganaizesheni, Issa Haji Gavu akielezea umuhimu wa wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la wapiga kura.
Dk Nchimbi akizungumza na wananchi wakati wa mapokezi yake
IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA
0754264203
No comments:
Post a Comment
ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇