Mwenyekiti
wa Jumuiya ya Wanawake (UWT) Mkoa wa Dar es salaam Ndugu. Mwajabu
Rajabu Mbwambo, ameshiriki katika kongamano la "_Thamani ya Bint
Mwenye Ndoto 2024_" lililoandaliwa na asasi isiyo ya serikali Voice of
Eagle Tanzania chini ya CEO wa Bwana Meshack Mafyeko. Katika
Kongamano Komredi Mwajabu ametoa Mada Fursa ya Bint mwenye ndoto na
Uongozi. Mada hiyo imegusa nukta zifuatazo:
Sifa za kiongozi
1. Awe na ufahamu katika maeneo yafuatayo;
- Taasisi/ kikundi
biashara anayoongoza
- Malengo
- Mipango
- Maono
-Mazingira
- Fursa
- Changamoto
2. Awe na hofu ya mungu na kutenda majukumu yake kwa uadilifu.
3. Awe na maadili mema. Asigombanishe, kufitinisha, umbeya, majungu, chuki, wivu na mwizi.
4. Awe mwaminifu
5. Uwezo wa kujifunza kila mara, kuongeza ufanisi wake na kujifunzs kwa waliofanikiwa
6. Awe Mstahamilivu/ Resilience
7. Kupokea ushauri na kushauri
*Cde
Mwajabu* amewajuza kwamba ili kufikia Malengo ni lazima kujiendeleza
wao binafsi kwa kupata mbinu za kuongoza kwa kuangalia yafuatayo;
1. Kutambua vipawa walivyo navyo na madhaifu yao ili kujiboresha na kuwa weled zaidi
2. kufahamu aina ya uongozi kulinga na eneo walilojikitana nalo
3. kutengeneza na kutanua wigo wa networking.
4. kuwa Role Model wa kujifunza na kupata ushauri wake
5. wahakikishe kila siku wanajifunza mbinu na mikakati ya uongozi.
Cde
Mwajabu amewapa mfano mzuri kwa Tanzania Role Model aliyepo Madarakani
Rais *Dr Samia Suluhu Hassan* na falsafa ya 50/ 50 na amehakikisha
ameweka mawaziri na manaibu wanawake, makatibu na manaibu katibu wa kuu
wanawake, wakuu wa mikoa na wilaya na makatibu tawala mikoa na wilaya,
wakurugenzi na viongozi mbalimbali wanawake katika taasisi za serikali.
Cde.
Mwajabu amepongeza Rais Dr Samia Suluhu Hassan kwa mambo mengi
aliyofanya ndani ya kipindi cha miaka mitatu kwa kuwa kiongozi bora wa
kuacha alama na kusimamia falsafa yake ya 4Rs
na kunyanyua wanawake wenye uwezo kwa kuwateua katika nafasi za juu za uongozi ili kuleta mabadiliko.
"Binti unatakiwa ujipambanue kwa kujitambua kuwa Personal Branding yako ni
1. Tabasamu lako ndio Logo yako
2. Muonekano wako ndio Business Card yako
3. Jinsi unavyofanya wengine wajisikie katika uongozi wako ndio Trade mark yako".
Ndugu. Mwajabu Mbwambo
Mweyekiti wa UWT Mkoa wa Dar es salaam.
Ubungo Mlimani City
23 Machi, 2024
#Thamani yabinti mwenye Ndoto 2024
#Dar es salaam
# UwtImara Jeshi la Mama Kazi iendelee
| |||





No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇