Furaha kumpokea Naibu Waziri wa Nishati Ndg. Judith Kapinga na ujumbe wa Kamati ya Bunge inayosimamia Nishati ukiongozwa na Cde. Mathayo David kwenye Halmashauri yetu ya Chalinze. Ziara yao imeleta mafanikio makubwa sana. Kamati imeona jinsi Nishati ya umeme ilivyotandazwa kila sehemu. Chalinze imefikiwa kwa 100% na nishati ya umeme; kila kijiji kimefikiwa, Shule zetu za Msingi 96%, Sekondari 98%, Nyumba za Ibada 98%, Miji yetu mikubwa bado 2 tu etc. Kazi sasa ni usambazaji na kuunganisha wateja wapya. Asante Rais wetu Samia Suluhu Hassan kwa hili nalo. Kweli wewe ni mtu wa Kazi. #KaziIendelee


No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇