LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Dec 11, 2023

CHATANDA: WATENDAJI UWT ONGEZENI UFANISI KAZINI, TUSHINDE CHAGUZI ZIJAZO

 

Katibu Mkuu wa UWT, Jokate Mwegelo akiwahamasisha washiriki alipokuwa akizungumza maneno ya utangulizi kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa UWT, Chatanda kuyafungua mafunzo hayo.

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tganzania (UWT), Mary Chatanda (katikati), Katibu Mkuu wa UWT, Jokate Mwegelo (kushoto) na Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi 2022, Spika mstaafu Anne Makinda wakiwa na furaha huku wakipiga makofi wakati wa ufunguzi wa semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo na uelewa watendaji wa UWT kutoka mikoa ya Tanzania Bara na Visiwani pamoja na makada wa CCM kwenye Ukumbi NEC-CCM (White House) jijini Dodoma Desemba 11, 2023.

Chatanda ametoa rai kwa watendaji  hao kuyatumia mafunzo hayo kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku na wahakikishe wanajiandaa kushinda uchaguzi ujao wa serikali za mitaa na kuongeza idadi ya wanachama watakao mpatia ushindi mkubwa  Rais Samia Suluhu Hassan katika uchaguzi mkuu 2025.


Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Dodoma, Neema Majule akitoa salamu za mkoa huo pamojana kuwakaribisha watendaji hao mkoani humo.
Washiriki wa semina hiyo wakiwa na furaha wakati wa kutambulishwa wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Martha Mlata akiongoza kuimba wimbo wa hamasa.
Ni hamasa kwa kwenda mbele kwa kila kundi la washiriki kutoa kibwagizo cha mkoa wanaotoka.




















IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA

0754264203





 

No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages