Na Richard Mwaikenda, Mlele
Katibu Mkuu wa CCM, Komredi Daniel Chongolo ameshitukia kusuasua kwa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami ya Kibaoni-Stalike hivyo kuagiza uongozi wa wilaya ya Mlele ukiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Mlele, Majid Mwanga kukutana na uongozi wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Kampuni ya ushauri na mkandarasi Ili kuhakikisha kasi ya ujenzi inaongezeka.
Chongolo ametoa agizo Hilo baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo iliyopo wilayani Mlele, Katavi Oktoba 4,2023, wakati wa ziara ya kuimarisha uhai wa chama, kusikiliza kero za wananchi na kukagua utekelezaji wa Ilani ya chama hicho.
Wakati wa kuhitimisha ziara yangu Oktoba 7, 2023, nitamuita Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa aje kukagua Maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo na kuwaeleza wananchi ni namna gani barabara hiyo itakamilishwa kwa spidi."
Barabara hiyo yenye urefu wa zaidi ya Km 50 inayogharimu zaidi sh. Bil. 80, inajengwa na Kampuni ya China ya CRSG. Ujenzi wa barabara ulianza Juni 23, 2022 na inatakiwa ukamilike Juni 22, 2925.
Akitoa taarifa kwa Katibu Mkuu wa CCM, Chongolo, Kaimu Meneja wa TANROADS Mkoa wa Katavi, Albert Laizer kuhusu Maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo, amesema kuwa umefika asilimia 11.2 nyuma ya utekelezaji ambao ulipaswa uwe asilimia 21. Muda umefika miezi 15 kati ya 36 iliyopangwa. Hadi sasa mkandarasi ameshalipwa kianzio zaidi ya sh. Bil. 12.






No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇