LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 3, 2023

CHONGOLO: AMTAKA WAZIRI BASHUNGWA KUPELEKA SHEREHE ZA KUSAINI MKATABA YA UJENZI WA BARABARA YA LAMI BANDARI YA KAREMA

Katibu Mkuu wa CCM, Komredi Daniel Chongolo akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Bandari za Ziwa Tanganyika, Edward Mabula kuhusu Bandari ya Karema alipokagua Bandari hiyo iliyopo Wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi Oktoba 3, 2023.

Chongolo ameiagiza Serikali kujenga haraka barabara ya lami inayokwenda katika Bandari hiyo iliyojengwa kwa gharama ya sh. Bil. 49. 


Aidha amemtaka Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa sherehe za kuingia mkataba wa ujenzi wa barabara hiyo zifanyike eneo la bandari hiyo ili wananchi wa eneo hilo nao washuhudie.

Bandari hiyo itakuwa inahudumia pia Shehena za mizigo za nchi jirani za DRC Congo, Burundi na Zambia..






Chongolo akisalimiana na mmoja wa abiria katika Bandari ya Karema

Akikagua eneo la bandari hiyo

Mbunge wa Mpanda Vijijini, Selemani Kakoso akielezea umuhimu wa ujenzi wa barabara ya lami ya kwenda kwenye bandari hiyo.

 IMEANDALIWA NA RICHARD  MWAIKENDA 

No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages