LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Aug 11, 2023

RAIS DK. SAMIA AWAPANGIA VITUO MABALOZI ALIOWATEUA, WANNE AWABADILISHA VITUO, DK. NCHIMBI KUREJEA NYUMBANI

Na Bashir Nkoromo, CCM Blog.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan, amewapangia vituo vya kazi Mabalozi aliowateua Mei 10, 2024 na kuwabadilisha vituo vya kazi Mabalozi wanne.

Taarifa ya Ikulu imewataja Mabalozi waliopangiwa vituo vya kazi ni Balozi Fatma Mohd Rajab aliyepangiwa Oman badala ya Balozi Aabas Kilima anayestaafu na Balozi Joseph Edward Sokoine nchini Canada badala ya Dk. Mpoki Ulisubisya anayestaafu, huku Balozi Naim Sweetie Hamza Aziz akipangiwa nchini Australia.

Taarifa imesema, Rais amemteua kuwa Balozi Meja Jenerali Ramson Godwin Mwasika na kumpangia kwenda nchini Rwanda, badala ya Meja Jenenerali  Richard Mutayoba Makanzo aliyehamishiwa Cairo, Misri na kumteua kuwa Balozi Gelastus Gasper Byakanwa kisha kumpangia kwenda Burundi badala ya Jilly Maleko liyestaafu.

Rais amemteua pia kuwa Balozi Habibu Awesi Mohamed na kumpangia kwenda Qatar badala ya Balozi Mahadh  Juma Maalim  aliyemhamishia Kuala Lumpur, Malaysia na kumteua Imani Salum Mjalikali kisha kumpangia kwenda Algeria badala ya Meja Jenerali Jacob Gideon Kingu aliyestaafu.

Pia Rais amemteua kuwa Balozi Hassan Iddi Mwamweta na kumpangia kwenda Ujerumani  badala ya Abdallah Salehe Possi aliyemhamishia Geneva Uswisi pia Rais akimteua kuwa Balozi Dk Mohamed Juma Abdallah na kumpangia Saud Arabia badala ya Balozi Ali Jabir Mwadini  anayeenda  Paris, Ufaransa.

Taaraifa imewataja waliohamishwa vituo kuwa ni,  Balozi Ali Jabir Mwadini aliyehamishiwa Ufaransa, badala ya Balozi Dk. William Shelukindo aliyeteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya mambo ya Nje na Usgirikiano wa Afrika Mashariki.

Aidha Balozi Meja Jenerali Richard Mutayoba Makanzo Rais amemhamishia kwenda Misri badala ya Balozi Dk.  John Emmanuel Nchimbi anayerejea nyumbani, huku Balozi Abdallah Possi akimhamisha kwenda kuwa Mwakilishi wa Kudumu Ofisi za Umoja wa Mataifa (UN) Geneva Uswisi badala ya Maimuna Tarishi aliyemaliza mkataba.

Taarifa imekamilisha ikisema Balozi Dk. John Stephen Simbachawene amehamishiwa nchini Uganda badala ya Balozi Azizi Mlima anayestaafu na kwamba Mabalozi wateule wataapishwa Agosti 15, 2024 saa 5 asubuhi. Ikulu, Chamwino, Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages