LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Apr 1, 2023

MLATA AMPONGEZA RAIS DK. SAMIA KUJALI MICHEZO NCHINI

 MLATA AMPONGEZA RAIS DK. SAMIA


Na HEMEDI MUNGA

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida, Martha Mlata amempongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutekeleza Ilani ya chama hicho katika sekta ya michezo.

Mlata anamshukuru Rais Dk. Samia kwa kuhamasisha michezo kwa kutoa fedha kuzipatia timu za Simba, Yanga na Taifa Stars katika kila goli wanalofunga katika michuano ya kimataifa inayoshiriki timu hizo.

Akizungumza hivi karibuni na waandishi wa habari  punde baada ya kukagua uwanja wa Liti mkoni hapo baada ya kiwanja hicho kuchaguliwa kutumika katika michuano ya Shirikisho la Azam Federation Cup  Nusu Fainali, Mwenyekiti huyo anasema Rais Dk. Samia katoa fedha kwa wanamichezo kwa lengo la kuendelea kutekeleza resa za chama hicho katika michezo.

‘’Tunamshukuru sana Rais DK. Samia hakika yeye ni mdau mkubwa sana wa michezo,’’ anashukuru.

Aidha, anasema kutokana na fursa hizo na nyingine, wao wanahamasisha michezo shuleni kwa lengo la kuhakikisha wanaendelea kuibua vipaji, waliyo na vipaji kuwaunganisha na fursa mbalimbali.

Kuelekea michuano hiyo ya nusu fainali ya kombe la Azam Federationi Cup, Mwenyekiti huyo anasema ujio wa timu hizo ni fursa kwa wananchi wa mkoa huo kwa sababu watafanya biashara mbalimbali.

‘’Tumepokea kwa furaha sana kuwa uwanja wetu kuteuliwa kuwa moja ya viwanja  vitakavyochezewa nusu fainali ya michuano ya Shirikisho la Azam Federation Cup,’’ anashukuru.

Aidha, Mlata analishukuru Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa kulichagua dimba la Liti litumike katika michuano hiyo.

‘’Hakika tunafahamu viwanja vipo vingi ambavyo ni vizuri lakini TFF wameuchugua uwanja wetu wa Liti, tunawashukuru sana,’’

Kutokana na ofa hiyo, Mlata anamshukuru Meneja wa uwanja huo kwa sababu ameendelea kuutunza hasa namna pichi yake inavyoonekana katika sura nzuri.

Anasema hakika Meneja huyo anafanya kazi nzuri sana ambayo imewezesha TFF kuuchagua uwanja huo, hivyo amefanikiwa kuupa sifa mkoa huo.

‘’ Kwa kweli wananendelea kutupa raha, sifa na heshima kwa sababu kazi anayoifanya Meneja inaonekana na ndio maana TFF wameuchugua,’’ anasema.

Halikadhalika, anasema ni fursa kwa wajasiriamali na wafanyabiashara wa mkoa huo kufanya biashara ikiwemo katika nyumba za kulala wageni.

Anasema mkoa huo una malighafi nyingi zikiwemo mahindi, karanga, asali, vitunguu, kuku wa kienyeji, mayai na mafuta ya alizeti.

Kwa upande wa Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Soka mkoa wa Singida amabye ni Diwani wa kata ya Kindai (SIREFA), Omary Hamisi anasema itakuwa ni heshima kwa mkoa huo kama timu ya Singida Big Star itaingia nusu fainali ya michuano hiyo.

Aidha, anawahakikishia wapenzi na washabiki wa soka Tanzania kuwa timu yao itasonga mbele katika michuano hiyo.

Michuano ya kome la Shirikisho la Azam Federation Cup inatarajia kitimua vumbi April 7 na 8 mwaka huu.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida, Martha Mlata akizungumza hivi karibuni na waandishi wa habari  punde baada ya kukagua uwanja wa Liti mkoa wa Singida baada ya kiwanja hicho kuchaguliwa kutumika katika michuano ya Shirikisho la Azam Federation Cup  Nusu Fainali.(Picha kwa hisani ya ofisi ya chama)

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida, Martha Mlata akikagua uwanja wa Liti. (Picha kwa hisani ya ofisi ya chama)


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida, Martha Mlata akikagua pichi ya uwanja wa Liti. (Picha kwa hisani ya ofisi ya chama)



No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages