Mbunge wa jimboni la Chalinze na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makzi, Ridhiwani Kikwete, Februari 16, 202 aimegawa pikipiki kwa watendaji wa kata 6 za Halmashauri yetu ya Chalinze, kutembelea kiwanda cha Uzalishaji wa marumaru cha Keda, na kupokea vifaa tiba kwa ajili ya Vituo Vya Afya Viwili Kata za Kibindu na Msata na Zahanati vijiji 11.
Wakati akikabidhi pikipiki, amewakumbusha Watendaji kutumia vifaa hivyo kuzingatia makusudio ya kutolewa kwake. Wakawasikilize wananchi na kutoa ufumbuzi wa changamoto zao.
"Tukikabidhi vifaa tiba tumewahimiza kuvitunza na kuvitumia kwa makusudio yake. Kazi kubwa inaelekezwa kituo cha Afya Miono ambapo kazi ya ujenzi wa miundo mbinu inapaswa kuwa kipaumbele. Kwa upande wa kiwanda tumewashukuru wawekezaji kwa kutambua mchango wa Mh. Raisi Dkt. Samia SuluhuHassan" #KaziInaendelea
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇