LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Feb 18, 2023

DC MWENDA AMPONGEZA RAIS DK. SAMIA KUPELEKA VIFAA VYA MATIBABU KITUO CHA AFYA MONDULI .

 Wananchi Engaeuka Monduli wafurahia kituo cha Afya. 

MKUU wa wilaya ya Monduli jijini Arusha, Suleiman Mwenda amefanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo, kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

Mwenda alisema anafanya hivyo kwa sababu Rais Dk. Samia Suluhu Hassan alitoa fedha nyingi katika idara ya afya kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanapata matibabu karibu na maeneo wanayoishi.

Akizungumza na wananchi jana wakati alipotembelea mradi wa kituo cha afya kata ya Engaruka wilayani hapo, Mwenda aliwataka wananchi kuendelea kuiunga mkono serikali kwa sababu inawajali.

‘’ Ndungu zangu Rais Dk. Samia alileta fedha nyingi sana, hivyo ni wajibu watu kusimamia miradi hii ikamilike kwa wakati na iwe na samani ya fedha,’’ alisema.

Aidha, alisisitiza kuwa ujenzi unatakiwa kukamilika haraka kwa sababu Halmashauri hiyo imeshapokea vifaa vyenye thamani ya sh 400 milioni vitakavyotumika katika kituo hicho cha Afya.

Akisoma taarifa fupi mbele ya mkuu huyo wa wilaya Kaimu Mganga mkuu wa Hospitali iliyopo katika Halmashauri hiyo, Constantine Rahi alisema wanaweka nguvu kuhakikisha maagizo ya mkuu huyo wa wilaya yanatimia kwa wakati.

‘’ Hadi hivi sasa ujenzi wa kituo cha Afya umeishagharimu kiasi cha sh 188 milioni kukamilisha jengo la upasuaji na maabara, hivyo ninaamini tutakamilisha kwa wakati,’’ alisema.

Aliwahakikisha wananchi kuwa serikali imewaletea vifaa vitakavyotumika katika kituo hicho, hivyo wamejipanga kuwahudumia wananchi kutimiza malengo ya serikali.

Kwa upande wao wananchi waliofurika katika ziara hiyo wa walimshukuru Dk. Samia kwa sababu amewaletea huduma hiyo karibu.

Joyce Joseph alisema huduma ya afya walilazimika kuifuata umbali wa kilometa 60 kwenda Mto wa Mbu kutoka katika makazi waliokuwa wanaishi.

‘’ Ilikua ni adha na azabu kufuta huduma mbali, tunamshukuru Rasi Samia kutusogezea huduma hii karibu hakika Mungu ndie anaweza kumlipa badala Rais wetu,’’ alisema.

Mkuu wa wilaya ya Monduli anaendelea na ziara ya kutembelea takribani kata 18 za wilaya hiyo kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

Hatua hiyo ni utekelezaji wa maagizo ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ya kuhakikisha falsafa ya Rais Dk. Samia kuwahudumia wananchi inatimia kikamilifu.


MKUU wa wilaya ya Monduli jijini Arusha, Suleiman Mwenda akitembelea ujenzi wa kituo cha afya kata ya Engaruka wilayani hapo leo, kulia kwake ni Kaimu Mganga mkuu wa Hospitali iliyopo katika Halmashauri hiyo, Constantine Rahi. (Picha kwa hisani ya ofisi ya mkuu wa wilaya)
MKUU wa wilaya ya Monduli jijini Arusha, Suleiman Mwenda akitembelea ujenzi wa kituo cha afya kata ya Engaruka wilayani hapo leo, kulia kwake ni Kaimu Mganga mkuu wa Hospitali iliyopo katika Halmashauri hiyo, Constantine Rahi. (Picha kwa hisani ya ofisi ya mkuu wa wilaya)


MKUU wa wilaya ya Monduli jijini Arusha, Suleiman Mwenda akitembelea ujenzi wa kituo cha afya kata ya Engaruka wilayani hapo leo, kulia kwake ni Kaimu Mganga mkuu wa Hospitali iliyopo katika Halmashauri hiyo, Constantine Rahi na baadhi ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). (Picha kwa hisani ya ofisi ya mkuu wa wilaya)

MKUU wa wilaya ya Monduli jijini Arusha, Suleiman Mwenda akitembelea ujenzi wa kituo cha afya kata ya Engaruka wilayani hapo leo, kulia kwake ni Kaimu Mganga mkuu wa Hospitali iliyopo katika Halmashauri hiyo, Constantine Rahi na baadhi ya viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM). (Picha kwa hisani ya ofisi ya mkuu wa wilaya)
MKUU wa wilaya ya Monduli jijini Arusha, Suleiman Mwenda akitembelea ujenzi wa kituo cha afya kata ya Engaruka wilayani hapo leo, kulia kwake ni Kaimu Mganga mkuu wa Hospitali iliyopo katika Halmashauri hiyo, Constantine Rahi. (Picha kwa hisani ya ofisi ya mkuu wa wilaya)
MKUU wa wilaya ya Monduli jijini Arusha, Suleiman Mwenda akitembelea ujenzi wa kituo cha afya kata ya Engaruka wilayani hapo leo, kulia kwake ni Kaimu Mganga mkuu wa Hospitali iliyopo katika Halmashauri hiyo, Constantine Rahi na baadhi ya viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM). (Picha kwa hisani ya ofisi ya mkuu wa wilaya)

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages