LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jan 10, 2023

WAZIRI JAFO: DUWASA HONGERENI, NYIE NDIYO MFANO WA KUIGWA UTUNZAJI WA MAZINGIRA DODOMA+video

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo ameupongeza uongozi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) kwa kuwa mstari wa mbele kushiriki kampeni za upandaji miti katika mkoa huo.

Jafo ametoa pongezi hizo mbele ya Mkurugenzi Mtendaji wa Duwasa, Eng. Aron Joseph alipokuwa akizungumza na wananchi wakati wa zoezi la la upandaji miti kando ya barabara jijini Dodoma leo Januari 10, 2023 ikiwa ni Wiki ya Maadhimisho ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.


 Mkurugenzi Mtendaji wa Duwasa, Eng. Aron Joseph akishiriki kazi ya upandaji miti  kando ya barabara jijini Dodoma leo Januari 10, 2023 ikiwa ni Wiki ya Maadhimisho ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Mdau, nakuomba uendelee kusikiliza kupitia clip hii ya video, Waziri Jafo akitoa pongezi hizo kwa DUWASA...

IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA 
MHARIRI BLOG YA TAIFA YA CCM 
0754264203

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages