LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jan 16, 2023

UONGOZI WA UWT TAIFA WAKUTANA NA RAIS MWINYI ZANZIBAR

 

Makamu Mwenyekiti CCM Zanzibar,Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi leo Jumatatu Januari 16,2023 amekutana na Viongozi wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Ikulu Zanzibar. 

 Uongozi wa Jumuiya hiyo uliongozwa na Mwenyekiti wa UWT Taifa Ndugu Mary Chatanda ,Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa aliyeambatana na Makamu Mwenyekiti UWT Zanzibar Ndugu Zainab Shomari ,viongozi mbalimbali wa kitaifa wa Jumuiya hiyo kwa nia ya kujitambulisha baada ya kuchaguliwa .

 Pia wamempongeza Dk.Hussein Ali Mwinyi kwa kuchaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti CCM Zanzibar na Kutekeleza Ilani ya CCM ya Utekelezaji 2020-2025 . CODE





Mwenyekiti wa UWT Taifa Ndg Mary Chatanda akikabidhi Tuzo ya Pongezi kwa Mhe Dkt Hussein Ali Mwinyi kwa kuchaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti CCM Zanzibar na Kutekeleza Ilani ya CCM ya Uchaguzi 2020-2025. #UWTImara #JeshiLaMama #KaziIendelee
Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Ali Mwinyi akiteta jambo na ujumbe waViongozi wa Umoja  wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa Ikulu Zanzibar mapema leo

Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Ali Mwinyi akiteta jambo na ujumbe waViongozi wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa Ikulu Zanzibar mapema leo
Ndg Mary Chatanda, Mwenyekiti wa UWT Taifa akiwa Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Ali Mwinyi mara baada ya mazungumzo


Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Ali Mwinyi akiwa kwenye picha ya pamoja na Makamu Mwenyekiti wa UWT Taifa Ndugu Zainab Shomari mara baada ya kuteta na Viongozi wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa Ikulu Zanzibar mapema leoujumbe ambao uliongozwa na Mwenyekiti wa UWT Taifa Ndugu Mary Chatanda.
Ndg Riziki Kingwande, Naibu Katibu Mkuu UWT - Bara





Mbunge Neema Lugangira: Mbunge Neema Lugangira akiwa kwenye picha ya pamoja na Makamu Mwenyekiti CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi leo Jumatatu   







No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages