LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jan 17, 2023

PROF. MUHONGO KUENDESHA HARAMBEE ZA KUCHANGIA UJENZI NA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA SEKONDARI ZA KATA

 

Jimbo la Musoma Vijijini lina Kata 21 zenye Vijiji 68 na Vitongoji 374.


Jimbo hili lina jumla ya Sekondari 27: 

*25 za Kata/Serikali

*2 za Binafsi

(SDA & KATOLIKI)


UPUNGUFU WA MIUNDOMBINU


Tunaendelea na ujenzi na uboreshaji wa miundombimu iliyopungufu kwenye Sekondari zetu za Kata.


Bado kuna mahitaji ya maabara, maktaba, vyumba vya madarasa, ofisi za walimu (majengo ya utawala), vyoo, nyumba za walimu, n.k. kwenye Sekondari zetu za Kata.


Vilevile, kuna matatizo ya wanafunzi kutembea umbali mrefu kwenda masomoni, na mirundikano ya wanafunzi madarasani (wingi wa watoto wanaopaswa kwenda sekondari) - tunalazimika kuongeza idadi ya sekondari kwenye baadhi ya kata zetu.


Tunashukuru sana Serikali yetu, chini ya uongozi wa Rais wetu, Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan, kuendelea kuchangia ujenzi na uboreshaji wa miundombimu iliyotajwa hapo juu.


HARAMBEE ZA MBUNGE WA JIMBO


Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo, ataendesha HARAMBEE MBILI kwa ajili ya ujenzi na uboreshaji wa miundombinu ya elimu kwenye SEKONDARI MBILI.


(1) BWAI SEKONDARI


Hii ni Sekondari mpya na ya pili ya Kata ya Kiriba ambayo imefunguliwa wiki iliyopita. Mategemeo ni kuwa na Wanafunzi 150 wa Kidato cha kwanza (Form I)


Harambee Bwai Sekondari

*Alhamisi, 19.1.2023

*Saa 9 alasiri (15 hrs)


Michango ipelekwe kwa:

*Headmaster

  0757 471 516

  0612 409 257


(2) MUHOJI SEKONDARI


Sekondari hii inajengwa kwenye Kata ya Bugwema yenye vijiji vinne (4), na ambayo ni kubwa (eneo) kuzidi Kata zetu zote.


Hii itakuwa Sekondari ya pili ya Kata ya Bugwema


Harambee Muhoji Sekondari

*Jumanne, 24.1.2023

*Saa 8 mchana (14 hrs)


Michango ipelekwe kwa:

*Mtendaji wa Kijiji (VEO)

 0686 557 264


*MICHANGO inaombwa kutoka kwa Wazaliwa wa Musoma Vijijini na hasa wa kutoka maeneo yenye miradi hiyo, na Wadau wengine wa Maendeleo -  KARIBUNI SANA!


Ofisi ya Mbunge

Jimbo la Musoma Vijijini

www.musomavijijini.or.tz


Tarehe:

Jumanne, 17.1.2023

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages