LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jan 31, 2023

MHAGAMA ATAJA TAASISI ZINAZOONGOZA KWA UVUNJIFU WA MAADILI KATIKA UTUMISHI WA UMMA

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora Mhe.Jenista Mhagama,akisisitiza jambo kwa washiriki wakati akifungua kikao cha kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya maadili na utawala bora kilichofanyika leo Januari 30,2023 jijini Dodoma.

- Advertisement -

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora Bw.Xavier Daud,akizungumza wakati  wa kikao cha kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya maadili na utawala bora kilichofanyika leo Januari 30,2023 jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Usimamizi Maadili kutoka, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora Bi.Leila Mavika,akitoa utangulizi wa kikao cha kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya maadili na utawala bora kilichofanyika leo Januari 30,2023 jijini Dodoma.

   

- Advertisement -

Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora Mhe.Jenista Mhagama (hayupo pichani),wakati akifungua kikao cha kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya maadili na utawala bora kilichofanyika leo Januari 30,2023 jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Idara ya Mipango  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora Bw.Cosmas Ngangaji,akitoa neno la shukrani kwa mgeni rasmi (hayupo pichani) mara baada ya kufungua  kikao cha kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya maadili na utawala bora kilichofanyika leo Januari 30,2023 jijini Dodoma.

- Advertisement -

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora Mhe.Jenista Mhagama,akiwa katika picha ya pamoja na waandishi wa habari mara baada ya kufungua kikao cha kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya maadili na utawala bora kilichofanyika leo Januari 30,2023 jijini Dodoma.

   

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora Mhe.Jenista Mhagama,akiwa katika picha ya pamoja na washiriki mara baada ya kufungua  kikao cha kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya maadili na utawala bora kilichofanyika leo Januari 30,2023 jijini Dodoma.


HOTUBA YA MHE. JENISTA JOAKIM MHAGAMA (MB.), WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA KUHUSU MATOKEO YA TAFITI YA HALI YA UZINGATIAJI MAADILI KATIKA UTUMISHI WA UMMA YA MWAKA 2022, KWENYE KIKAO KAZI CHA WADAU WA USIMAMIZI WA MAADILI KATIKA UTUMISHI WA UMMA KATIKA UKUMBI WAKAMBARAGE, DODOMA TAREHE 30 JANUARI, 2023

 

Dkt. Laurean J. P. Ndumbaro - Katibu Mkuu, Ofisi ya

Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na

Utawala Bora;

Wakurugenzi wa OR - MUUUB;

Wakurugenzi wa Taasisi Simamizi za Maadili;

Wawakilishi wa Watendaji wa Bunge la Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania;

Mahakama na Jeshi la Polisi Tanzania;

Mameneja na Wakurugenzi wa Utawala na

Rasilimaliwatu;

Washiriki wa Kikao Kazi cha Wadau;

Watumishi wa OR - MUUUB mliopo hapa;


Waandishi wa Habari mliopo hapa;

Mabibi na Mabwana.

“Ninawasalimu kwa Jina la Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania”.

Ndugu Viongozi; Awali ya yote napenda kumshukuru

Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema kutujalia uzima

na kutuwezesha kukutana hapa siku ya leo tukiwa na

afya njema tukijiandaa kupokea Matokeo ya Tafiti ya

Hali ya Uadilifu katika Utumishi wa Umma ya

Mwaka 2022.

Kipekee nichukue nafasi hii kuwashukuru kwa utayari

wenu wa kushirikiana na Ofisi hii katika jukumu la

kuimarisha masuala ya Kiutumishi na Utawala Bora

kila inapohitajika. Hii inaonesha dhamira yenu ya

kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita

inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu

Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,

katika kuhakikisha tunakuwa na Utumishi wa Umma

3

wenye nidhamu, uwajibikaji wa hiari na utendaji wenye

matokeo kwa ustawi wa Taifa letu.

Ndugu Viongozi; Ofisi ya Rais, Menejimenti ya

Utumishi wa Umma pamoja na majukumu mengine ya

kusimamia Uendelezaji Sera katika Utumishi wa

Umma, Utawala wa Utumishi wa Umma, Usimamizi wa

Rasilimaliwatu na Mishahara, Usimamizi wa Mifumo ya

TEHAMA ya Uendeshaji wa Serikali, Usimamizi wa

Mifumo ya Utendaji Kazi wa kila Siku Serikalini,

Uendelezaji Rasilimaliwatu, Usimamizi wa Serikali

Mtandao na Usimamizi wa Anuai za Jamii katika

Utumishi wa Umma, pia ina jukumu la KUSIMAMIA

MAADILI YA UTENDAJI KATIKA UTUMISHI WA

UMMA NCHINI.

4

Ndugu Viongozi; Mtakumbuka kuwa mnamo mwezi

Desemba 2022, tukiwa katika kilele cha maadhimisho

ya wiki ya Maadili na Haki za Binadamu kitaifa, moja

ya mambo muhimu tuliyoyafanya OR MUUUB ilikuwa

ni kutoa taarifa ya muhtasari wa matokeo ya “Utafiti

wa Hali ya Uzingatiaji wa Maadili katika Utumishi

wa Umma nchini kwa mwaka 2022” (Public Service

Integrity Survey 2022). Utafiti huu ambao ulifanyika

katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 uliongozwa na

Mtaalam Mwelekezi kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe,

Kampasi ya Dar es Salaam kwa niaba ya OR MUUUB

ili kuweza kupata maoni huru. Utafiti huu umefanyika

kwa kutumia mbinu mbalimbali ikiwemo hojaji.

Ndugu Viongozi; Sote tunatambua kwamba Taasisi

za Umma ndio msingi mkubwa wa ufanisi katika

utekelezaji wa majukumu na mipango ya Serikali ya

kukuza uchumi, kutoa huduma bora kwa jamii na

kulinda amani na utulivu.

5

Taasisi hizo zimeundwa kwa ajili ya kufanikisha

jukumu la msingi la Serikali la kuleta ustawi kwa

Wananchi. Hivyo, ni wajibu wa Taasisi za Umma

nchini kuhakikisha zinafanikisha kufikiwa kwa malengo

ambayo Serikali imejiwekea Kitaifa na Kimataifa.

Malengo hayo ambayo Serikali imejiwekea

hayataweza kufikiwa endapo tutashindwa kuzingatia

na kusimamia vyema Maadili ya Utendaji katika

Utumishi wa Umma. Kwa kuzingatia hilo na dhamana

ambayo nimepewa na Serikali ya Awamu ya Sita

kusimamia masuala yote ya Utumishi wa Umma na

Utawala Bora, Ofisi yangu imekuwa ikitoa miongozo ya

Uzingatiaji wa Maadili ya Utendaji katika Utumishi wa

Umma; kuwajengea uelewa wa masuala ya Maadili ya

Utendaji Watumishi wa Umma na Wananchi; na

kufanya Ufuatiliaji wa Uzingatiaji wa Miongozo hiyo.

6

Utafiti ni moja ya njia zinazotumiwa na Ofisi yangu

kutathmini Hali ya Uzingatiaji wa Maadili ya Utendaji ili

kuiwezesha Serikali kufahamu hali ya Maadili katika

Taasisi zake na kutumia mrejesho huo kutambua na

kufanyia kazi maeneo ambayo yana

kasoro/mapungufu ili kuimarisha utoaji wa huduma

kwa wananchi.

Ndugu Viongozi; Tathmini ya Hali ya Uzingatiaji

Maadili zinazofanyika katika Utumishi wa Umma

zinalenga kupata taarifa sahihi za usimamizi wa

Maadili ya Utendaji na Maadili ya Kitaaluma Katika

Utumishi wa Umma. Ili kuimarisha usimamizi wa

Maadili katika Utumishi wa Umma, katika mwaka wa

fedha 2021/2022 Ofisi hii iliendesha Utafiti wa Hali ya

Uzingatiaji wa Maadili katika Utumishi wa Umma wa

mwaka 2022 (Public Service Integrity Survey).

7

Lengo kuu ilikuwa ni kubaini endapo kumekuwa na

ongezeko la uzingatiaji wa viwango vya Maadili ya

Utendaji kwa Watumishi Umma.

Ndugu Viongozi; Kama ambavyo nilizungumza wakati

wa uzinduzi wa Tafiti hii, Tafiti ya kwanza ya Maadili

(Integrity Survey) katika Utumishi wa Umma ilifanyika

mwaka 2006 kwa lengo la kupata taarifa za msingi

kwa ajili ya kuweka kiwango cha uzingatiaji wa Maadili

(baseline information). Matokeo ya utafiti kwa mwaka

2005 yalionesha kuwa kiwango cha uzingatiaji wa

Maadili katika Utumishi wa Umma kilikuwa asilimia

56.4 (56.4%). Kiwango hiki ndicho kilichukuliwa na

kutumika kama “baseline” kwa kuwa awali hakukuwa

na utafiti wowote ambao uliwahi kufanyika kupima hali

ya uzingatiaji wa Maadili katika Utumishi wa Umma.

8

Mnamo mwaka 2014, ulifanyika utafiti mwingine ili

kufahamu endapo kumekuwa na ongezeko la

uzingatiaji wa viwango vya Maadili kwa Watumishi

Umma; na kubaini maeneo yenye mianya ya uvunjifu

wa Maadili kwa lengo la kuweka mikakati ya

uimarishaji inayoendana na matokeo halisi. Kwa

mwaka 2014 kiwango cha uzingatiaji wa Maadili

kiliongezeka toka 56.4% (ya mwaka 2005) hadi kufikia

asilimia 66.9 (66.9%).

Ndugu Viongozi; Utafiti wa mwaka huu wa 2022

umefanyika baada ya kipindi cha miaka minane (8)

kupita kutoka Tafiti ya mwisho iliyofanyika mwaka

2014. Lengo kuu la utafiti wa mwaka 2022 ilikuwa ni

kubaini kama kumekuwa na ongezeko la uzingatiaji

wa viwango vya maadili katika Utumishi wa Umma

(follow up study) ambapo Matokeo ya Utafiti wa Hali

ya Uzingatiaji wa Maadili katika Utumishi wa Umma

kwa mwaka 2022 yameonesha kuwa kiwango cha

9

uzingatiaji wa Maadili katika Utumishi wa Umma

kwa mwaka 2022 ni asilimia 75.9 (75.9%). Matokeo

haya yanaonesha kiwango cha uzingatiaji wa Maadili

katika Utumishi wa Umma kimeongezeka kwa wastani

wa asilimia 9.8 (9.8%) kwa mwaka 2022 ikilinganishwa

na 66.1% (ya mwaka 2014). Ongezeko hili la kiwango

cha Maadili linatokana na dhamira ya uongozi thabiti

wa Serikali Awamu ya Sita, inayoongozwa na Mhe.

Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu;

Programu za mabadiliko ya Kisekta na Taasisi

zenyewe; na utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa

Kupambana na Rushwa (NACSAP).

Ndugu Viongozi; Kwa mujibu wa matokeo ya taarifa

ya Utafiti huu, yapo maeneo ambayo bado yanahitaji

kuboreshwa / kutiliwa mkazo. Maeneo hayo ni pamoja

na:-

10

(i) Ufuatiliaji wa kila mara wa uzingatiaji wa kanuni za

maadili kwa watumishi wa umma;

(ii)Mafunzo endelevu kwa watumishi ambao wako

kazini; wale wanaoajiriwa kwa mara ya kwanza na

elimu kwa umma; na

(iii) Usimamizi wa uzingatiaji wa Maadili katika utoaji

wa huduma wakati wa majanga ya kitaifa kama vile

UVIKO-19 na majanga mengine mbalimbali

yanayotokea nchini.

Aidha, maeneo ambayo yameonekana kulalamikiwa

zaidi kutokana na kuwepo kwa viashiria vya kukithiri

kwa vitendo visivyo vya uadilifu ni pamoja na Jeshi la

Polisi; Mahakama; Manunuzi ya Umma, Mikataba; na

Huduma za Ardhi. Matokeo kuhusu maeneo ambayo

yamelalamikiwa zaidi kwa kiasi kikubwa

yanashabihiana na matokeo yaliyotolewa katika utafiti

wa kitaifa kuhusu Rushwa (National Governance and

11

Corruption Survey), utafiti ambao uliendeshwa na

TAKUKURU mwaka 2020, ambapo utafiti huo pia

ulibainisha kati ya Taasisi zinazolalamikiwa kuwa na

viashiria vya kujihusisha na vitendo vya rushwa ni

pamoja na Jeshi la Polisi; Mahakama; na Usimamizi

wa Ardhi.

Ndugu Viongozi; Tarehe 9 Desemba, 2022, wakati

wa uzinduzi wa matokeo ya utafiti huu kwa Umma

kupitia vyombo vya habari, nilitoa maelekezo katika

maeneo sita ya kufanyiwa kazi. Eneo la kwanza

ilikuwa ni kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - Menejimenti

ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kufanya kikao

kazi cha pamoja na wadau kwa ajili ya kufanya

majadiliano ya kina kuhusu matokeo ya utafiti huu na

kuja na mikakati ya ufuatiliaji wa uzingatiaji wa Maadili

katika sekta zote kulingana na matokeo.

12

Katibu Mkuu (UTUMISHI) ametekeleza maagizo haya

kwa kuandaaa mkutano huu kuhakikisha kuwa taarifa

ya Utafiti huu inawafikia. Hivyo niwaelekeze kupokea

taarifa hiyo ambayo itawasilishwa kwenu na Mtaalam

Mwelekezi; kuchambua kwa kina taarifa hiyo; na

kutoka na maazimio na mipango itakayowezesha

Serikali kuboresha Usimamizi wa Maadili ya Utendaji

katika Utumishi wa Umma.


Majadiliano yenu katika siku hizi mbili za kikao kazi

yazingatie mambo muhimu yafuatayo:-

(i) Kuweka mikakati ya kukuza Maadili inayoendana

na hali halisi;

(ii) Kubaini maeneo yenye changamoto za kimaadili

na kuishauri mamlaka ipasavyo;

(iii) kujitathmini kuhusu hali ya kimaadili ya

Watumishi wa Umma na kushauri hatua stahiki

13

kwa maeneo ambayo yameonekana kuwa na

mapungufu;

(iv) Kubaini maeneo ambayo yanafanya vizuri na

kuweka mikakati ya kuendelea kujiimarisha; na

(v) Kuendelea kuimarisha dhana ya ushirikishwaji

wa wananchi katika kuimarisha utendaji wa

Serikali kama moja ya misingi ya Utawala Bora.

Ndugu Viongozi; kwa kuwa kikao kazi hiki

kimeshirikisha Viongozi ambao wamepewa

dhamana ya kusimamia eneo la Maadili na Utawala

Bora katika Taasisi zao, nitumie fursa hii

kuwafahamisha maagizo mengine niliyoyatoa

tarehe 9 Desemba 2022 wakati wa uzinduzi wa

taarifa ya utafiti:-

(i) Taasisi Simamizi za Maadili na Utawala Bora

pamoja na Vyama vya Kitaaluma kuendelea

kushirikiana na OR - MUUUB kukuza Maadili na

14

kutumia matokeo haya kuimarisha mikakati ya

usimamizi katika maeneo yao;

(ii)Waajiri kuhakikisha wanatenga Bajeti ya mafunzo

ya Maadili na kuendesha mafunzo kwa watumishi

wa umma walio kazini na wale wanaoajiriwa. Kama

ambavyo mmesikia moja ya eneo ambalo

halikufanya vizuri ni eneo la mafunzo kwa

watumishi;

(iii)Waajiri kuhakikisha wanaweka na kuimarisha

mifumo ya utoaji wa mrejesho ndani ya Taasisi zao

ili kuendelea kutoa fursa kwa wananchi kukemea

vitendo vya ukiukwaji wa Maadili;

(iv)Waajiri kuendelea kutoa elimu kwa umma kupitia

njia mbalimbali ikiwemo Vyombo vya Habari na

Tovuti kuhusu haki na wajibu wa wananchi katika

kupata huduma bora katika Taasisi za Umma; na

15

(v) Viongozi na Watumishi wa Umma wote nchini

kufanya kazi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na

Taratibu zinazosimamia Utumishi wa Umma kwa

kuwa ndiyo nguzo kuu ya Maadili ya Utendaji katika

Utumishi wa Umma.

Ndugu Viongozi; Nichukue fursa hii tena

kuwapongeza watumishi wa umma pamoja na Taasisi

zote zilizofanya vizuri kwa mujibu wa utafiti huu, kwa

kuweza kuzingatia na kuyaishi maadili ya utendaji

katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Matarajio yangu ni kuwa washiriki wa mkutano huu,

mtafanya uchambuzi wa kina wa taarifa hii na kutoka

na maazimio ambayo yatasaidia kuimarisha hali ya

uadilifu katika Utumishi wa Umma na hatimaye kuwa

na Taasisi nyingi zaidi zinazofanya vizuri katika eneo

la Maadili.



No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages