LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Nov 18, 2022

NAIBU WAZIRI DKT NDUGANGE AKAGUA KITUO CHA AFYA VUNTA, SAME MASHARIKI

 






, Naibu waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Dkt. Festo Ndugange  akiwa na Mbunge wa Same Mashariki Mhe Anne kilango  akikagua majengo ya kituo cha Afya kata ya Vunta na kutoridhishwa na hadhi ya kituo hicho. 


Dkt. Ndugange amesema serikali imetoa milioni mia tatu za awali kujenga kituo kipya cha Afya vunta  ambacho kitajegwa na jengo la upasuaji na chumba cha kuhifadhia maiti.

Ameendelea kusema Pesa hizo zimetolewa na Raisi Samiha Suluhu Hassani kuhakikisha wananchi wa kata ya vunta wanapata Huduma bora ya Afya 

Wakati akiwa kwenye ziara hiyo amemshukuru Mhe Anne kilango kwa juhudi kubwa anazofanya kuwapambania wananchi wa jimbo lake akiwa bungeni.

Pia nakusema  amevutiwa na miradi mikubwa ya jimbo hilo ikiendelea vizuri   ujenzi wa Madasa  ya Shule ya Sekondary ya Mihamba na zahati kubwa ya kisasa ambayo imegharimu milioni mia tano za ujenzi  wake ikikaribia kukamilika hivi karibu.

Pia amesema serikali itashirikiana na Tarura kuhakikisha  barabara zote ambazo zinajegwa hili kuleta unafuu kwa wakazi wa vijiji vya Same Mashariki kakamilika kwa wakati 

 Naibu waziri Festo amewaomba wananchi wa jimbo la Same Mashariki kumuunga mkono Raisi Samiha Suluhu Hassani kwa kazi kubwa anayoifanya kuleta maendeleo kwa wananchi wake 

Mhe Anne kilango amesema anatoa shukran sana kwa Raisi Samiha Suluhu Hassani kwa kumpatia milion mia tatu kwa ajiri ya ujenzi wa kituo  cha Afya vunta ambacho alikisemea akiwa bungeni zaidi ya mara tatu na leo utejelezajiwake unakwenda kukamilia.

Pia ameendelea kusema lengo lake ni kuona wananchi wake hawapati tabu kwenye mahitaji muhimu kama Afya,Elimu, Maji, na barabara hili waweze kupitisha mazao yao kwa wepesi  zaidi na ataendelea  kuwapatia wananchi wake miradi tofauti wajikwamue kiuchumi  
 picha na Ashrack Miraji

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages