LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Sep 26, 2022

LAWAMA ACHAGULIWA KUWA MWENYEKITI MPYA UWT WILAYA YA TEMEKE

Na Chiristopher Lissa wa Gazeti la Uhuru
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania Wilaya ya Temeke  wamemchagua  Lawama Mohammmed Mikidadi  kuwa Mwenyekiti mpya wa umoja huo wilayani humo.

Katika uchaguzi huo  uliofanyika Dar es Salaam, nafasi hiyo  ilikuwa  na wagombea  watatu ambao ni  Lawama, Hanifa  Kitwana Kondo na  Rukia Kamal.

Msimamizi wa Uchaguzi  huo ambaye ni Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya  Kinondoni, James Mgego  amemtangaza  Lawama kuwa mshindi kwa kupata kura 333.

"Mgego amesema nafasi ya pili imechukuliwa na  Anifa Kitwana Kondo aliyepata kura 143, huku Rukia Kamal akipata kura sita, hivyo ninamtangaza  Lawama Mohammed  Mikidadi kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake  UWT Wilaya ya Temeke” akasema Mgego.

Akizungumza baada ya kutangazwa mshindi, Lawama amewashukuru wajumbe kwa  kumuamini  kushika wadhifa huo na kwamba yuko tayari kuutumikia umoja huo na Chama Cha Mapinduzi CCM na kuwaomba  wajumbe na wanachama  wa UWT na Chama kumpa ushirikiano.

Mbunge wa Viti Maalumu  Mariam Kisangi,  aliwashukuru  wajumbe kwa  kufanya uchaguzi huo kwa amani.

Mbali na nafasi hiyo ya Mwenyekiti pia UWT wilayani humo ilipata viongozi wapya katika nafasi ya Mjumbe wa MkutanoMmkuu wa Mkoa, Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa UWT  na wawakilishi wa Mkutano wa Baraza la  UWT Mkoa. 

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Wilaya ya TemekeLawama Mohamed, akizungumza katika Mkutano Mkuu wa umoja huo, baada ya kuchaguliwa katika uchaguzi uliofanyika katika Ukumbi wa Sabasaba, Dar es Salaam. Kushoto ni aliyekuwa Msimamizi wa uchaguzi huo James Magego, Mbunge wa Viti Maalumu, Jane Jerry na aliyekuwa Mwenyekiti wa uchaguzi huo ambaye ni Mbunge wa Viti Maalumu, Mariam Kisangi. (Picha na Christopher Lissa).

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT)  Wilaya ya Temeke, Lawama Mohamed akizungumza katika Mkutano Mkuu wa umoja huo, uliofanyika katika ukumbi wa Sabasaba,Dar es Salaam.

Zifuatazo ni picha Wajumbe wakipiga kura👇

==================================
Wasimamizi wakihesabu kura

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages