LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Sep 12, 2022

AG FELESHI AISHUKURU ALSF KUWAJENGEA UWEZO WATAALAMU WA NDANI

Na Mwandishi Maalum, Dodoma
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Jaji Dk. Eliezer Feleshi amesema  mataifa mengi ya Afrika yamekuwa yakipoteza kesi  nyingi katika mahakama za kimtaifa na mabaraza ya usuluhishi kutokana  Mawakili wao kutokuwa na umahiri wa kutosha  unaoendana na  kasi ya mabadiliko  ya kiuchumi na kimaendeleo.

Na kwa sababu hiyo amesisitiza haja na umuhimu kwa mawakili hao wa Serikali pamoja na wataalamu wengine wakiwamo  wachumi na manunuzi kujengewa uwezo na umahili na ubobevu wa kuweza kukabiliana na changamoto za dunia ya sasa.

Ameyasema hayo wakati alipokutana na kufanya  mazungumzo na  Bi. Aida Sylla na Bi. Manuela Dieng  ambazo ni wataalamu kutoka Taasisi ya Kimataifa ya The African Legal Support Facitility ( ALSF) Mazungumzo hayo yamefanyika  Katika  Ofisi ya Mwanasheria Mkuu iliyopo  katika Jengo la Bunge  Dodoma.

ALSF ipo chini ya Banki ya Maendeleo ya Afrika ( AfDB) yenye Makao yake Makuu Abidjani, Cote d’Ivoire. Na inato pamoja na mambo mengine ushauri wa kisheria katika  nchi za Afrika pamoja na  mafunzo ya  kuwajengea uwezo wataalamu katika nchi hizo.

Wataalamu hao wapo  Mkoani Dodoma kwaajili ya mafunzo mafupi ya kuwajengea uwezo, umahili na  ujuzi  adimu  wataalamu wakiwamo mawakili wa serikali katika  maeneo mbalimbali ya uwekezaji mkubwa ikiwamo eneo la  madini, mafuta na  gesi.

“Wataalamu  wetu hapa Tanzania na Afrika kwa ujumla wakiwamo wanasheria, wachumi na watu wa manunuzi  wanakabiliwa na  changamoto nyingi,tunahitaji  kuwajengea uwezo na umahili  wa mara kwa mara, Afrika  tunapoteza kesi nyingi kwasababu tunapungukiwa ujuzi na utaalamu wa kiwango cha kimataifa, nipende kutoka  shukrani zangu za dhati kabisa kwa ALSF kukubali ombi la Ofisi yangu  la kuja kutoa mafunzo huu ni mwanzo mzuri wa ushirikiano endelevu” akabainisha  Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Aidha amesema, amefurahishwa pia kwamba miongoni mwa wataalamu watakao shiriki mafunzo hayo  wapo kutoka Tanzania Visiwani kwa kile alichosema yapo masuala mtambuka yanayohusu pande mbili za Muungano  ambayo wataalamu wake wanapaswa kuwa na uelewa wa pamoja.

Naye Bi Manuela Dieng akizungumza kwa niaba ya mwenzake, amesema ALSF imefurahi kuja kutoa mafunzo  hayo na kwamba huo ni mwanzo na akamwomba Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Eliezer Feleshi kuainisha maeneo  zaidi  ambayo  anadhani  yanahitaji kujengewa uwezo.

Vile vile wameelezea kuridhishwa kwao na ushirikiano ambao wanaupata kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na kwamba wanaendelea  pia na majadiliano ya maeneo zaidi ya kuwajengea uwezo.

Baadhi ya Taasisi na  Wizara zinazoshiriki mafunzo hayo ni Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali,  Bunge, EWURA, PURA, Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Nishati, Wizara ya Madini, Kamisheni ya Madini   Ofisi ya  Mwanasheria Mkuu  Zanzibar.

 Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika mazungumzo na  wataalam  Bi. Aida Sylla na  Bi Manuela Dieng kutoka Taasisi ya Kimataifa ya African Legal Support Facility ( ALSF) wataalam hao wamekuwa na Mazungumzo na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambapo pamoja na mambo mengine wamejadiliana  namna ALSF itakavyosaidia kuwajengea uwezo na umahili wataalamu wakiwamo Mawakili wa Serikali katika maeneo mbalimbali  yenye uwekezaji mkubwa yakiwamo ya madini, gesi na mafuta.  Jumla ya wataalamu 40 watapewa mafunzo katika maeneo hayo ambayo  yanafadhiliwa na ALSF.
Bi Manuela Dieng kutoka ALSF ambayo ni Taasisi ya Benki ya Maendeleo ya Afrika yenye  Makao yake Makuu Abidjani Cote D'Ivoire  akiwa na  mtaalamu  mwenzake Aida Sylla ambao wapo nchini  kwaajili ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wataalamu kutoka sekta mbalimbali. ALSF kupitia wataalamu hao wamemwomba Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuainisha maeneo mengine ambayo wataalam wa ndani wanahitaji kujengwea uwezo.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe Jaji Eliezer Feleshi akiwa  katika picha ya pamoja na wataalamu kutoka ALSF pamoja na  Wataalamu kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali mara baada ya mazungumzo  yaliyofanyika Ofisi ya Mwasheria Mkuu wa Serikali katika Jengo la Bunge

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages