LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 30, 2022

MWANARIADHA WA TANZANIA ALPHONCE FELIX SIMBU ASHINDA MEDALI YA FEDHA MASHINDANO YA MADOLA JIJINI BIRMINGHAM UINGEREZA, LEO

Mwanariadha wa Timu ya Tanzania Alphonce Felix Simbu aking'ata medali yake ya Fedha kwa furaha baada ya kuitwaa kwa kuibuka mshindi wa pili mbio za marathon katika Michezo ya Jumuiya ya Madola jijini Birmingham, Uingereza, nyuma ya Victor Kiplagat wa Uganda.
Mwanariadha wa Timu ya Alphonce Felix Simbu akiwa na furaha kwa kutwaa medali ya Fedha baada ya kuibuka mshindi wa pili mbio za marathon katika Michezo ya Jumuiya ya Madola jijini Birmingham, Uingereza, nyuma ya Victor Kiplagat wa Uganda.
Mwanariadha wa Timu ya Tanzania Alphonce Felix Simbu akiwa na akiwa mkimbiaji mwenzake pia wa Timu ya Tanzania Hamisi Misai ambaye alimaliza mbio hizo akiwa katika kumi bora ya mashindano kwa kushika nafasi ya nane.
Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Dkt. Asha-Rose Migiro (Aliyeshika Bendera ya Taifa) akiwa na timu ya Taifa ya Riadha pamoja na mwanariadha Alphonce Felix Simbu baada ya kushinda medali ya Fedha kwa kuibuka mshindi wa pili mbio za marathon katika Michezo ya Jumuiya ya Madola jijini Birmingham, Uingereza, nyuma ya Victor Kiplagat wa Uganda leo. Mkimbiaji Hamisi Misai  (wa tatu kulia) alimaliza katika kumi bora ya mashindano hayo kwa kushika nafasi ya nane. Wa pili kutoka kushoto ni Failuna Matanga ambaye alimaliza mtu wa tano katika marathon ya wanawake wakati Jackline Sakilu (wa pili kulia) akimaliza mwishoni akichechemea kutokana na maumivu ya msuli aliyoyapata akiwa kilomita 17 tu ya mchuano huo. Hivyo alichechemea hadi akamaliza huku akishangiliwa sana na umati mkubwa wa watu uliokuwepo. Kushoto ni kocha mkuu Suleiman Nyambui na kulia ni kocha msaidizi Lwiza John. (Picha zote na Mpigapicha Maalum).

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages