LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 12, 2022

KIJIJI CHA CHIWONDO, CHAMWINO WAONESHA FURAHA YAO KWA MKURABITA KUANZA URASIMISHAJI ARDHI+video

Wananchi wa Kijiji cha Chiwondo, wilayani Chamwino, Dodoma wameeleza furaha yao kwa kuishukuru serikali kuteua Kijiji chao kuwekwa kwenye mpango wa kurasimisha ardhi yao utakaofanywa na Mpango wa  Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge nchini (MKURABITA) kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino, mkoani Dodoma.


Urasimishaji huo unaoongozwa na Meneja Urasimishaji Ardhi Vijijini wa MKURABITA, Anthony Temu utafanyika kwa siku 12, katika  kijiji hicho chenye vitongoji 8 ambavyo ni; Kawawa, Karume, Matanga, Ngutoto, Mkokani, Majengo, Chapakazi na Chikwama.


Meneja wa Urasimishaji Ardhi Vijijini wa MKURABITA, Anthony Temu akielezea kuhusu mpango huo katika kikao cha Halamashauri ya Kijiji hicho pamoja na maafisa wa Halamashauri ya wilaya hiyo.
Baadhi ya maafisa wa Hamashauri wakiwa katika kikao hicho cha maandalizi.
Baadhi ya wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji.
Mdau, nakuomba uendelee kusikiliza kupitia clip hii ya video, Anthony Temu akielezea kuhusu mpango huo wa urasimishaji  ardhi na wananchi wakielezea furaha yao...

IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA 
 MHARIRI BLOG YA TAIFA YA CCM 
 0754264203

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages