JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI - KAMPENI YA SENSA YA WATU NA MAKAZI
KAMPENI hiyo itafanywa ndani ya Kata zote 21 zenye Vijiji 68.
MUDA wa KAMPENI
Kuanzia tarehe 30.7.2022 hadi tarehe 22.8.2022
UZINDUZI
*Jumamosi, 30.7.2022
*Saa 9 Alasiri
*Kijijini Busekera
VIONGOZI watakaongoza Kampeni hiyo ni:
*Mkuu wa Wilaya
(Dkt Khalifan Haule)
*Mkurugenzi wa Halmashauri
(Ndg Msongela Palela)
*Mbunge wa Jimbo
(Prof Sospeter Muhongo)
VIKUNDI VYA UHAMASISHAJI vimetayarishwa na Mbunge wa Jimbo. Vikundi hivyo ni:
*Kwaya ya Bugoji
*Kwaya ya Kiriba
*Ngoma ya Liranda Bugwema
*Ngoma ya Kiwanjuki Kiriba
*Ngoma ya Mbegete Nyakatende
*Mtelezo Show ya Nyakatende
KIPEPERUSHI kimoja chenye kurasa/pande mbili (kimeambatanishwa hapa) kitagawiwa ndani ya Vijiji vyote 68.
JIANDAE KUHESABIWA
Tarehe 23.8.2022
Usisahau kutembelea TOVUTI ya Jimbo letu ambayo ni:
www.musomavijijini.or.tz
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz
Tarehe:
Jumanne, 26.7.2022
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇