Mbunge wa Singida Mashariki, Midraji Mtaturu amempongeza Rais Samia kuutangaza utalii kupitia filamu ya Royal Tour na kwamba tayari matokeo yameanza kuonekana. Aidha, Mtaturu, wizara husika ya Maliasili na Utalii kutobweteka kuunga mkono juhudi zilizofanywa na Rais Samia, bali wakaze buti kuhakikisha utalii unazidi kupaa. Pia kuboresha mambo mbalimbali yanayokwamisha watalii kuja nchini zikiwemo tozo na ukwasi kwenye viza. Ametoa pongezi hizo na ushauri huo alipokuwa aakichangia mjadala wa makadirio ya Bajeti ya wizara hiyo, Juni 3, 2022 bungeni Dodoma.
Mdau, nakuomba uendelee kusikiliza kupitia clip hii ya video, Mtaturu akitoa ushauri wake huo....
IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA MHARIRI BLOG YA TAIFA YA CCM
0754264203

No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇