Hayo yamesemwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana Jijini Dodoma wakati akizindua Mpango Kazi wa Kitaifa wa Usimamizi Shirikishi wa Misitu na Takwimu za usimamizi shirikishi wa Misitu ya Jamii.
Dkt. Chana alisema kuwa Tanzania inapoteza takribani hekta 469,000 za misitu kila mwaka akiongeza kuwa kama juhudi za pamoja hazitachukuliwa kuna hatari ya nchi kuanza kupata athari za kimazingira ambazo huathiri nchi yetu na dunia kwa ujumla.
Aidha, amewahimiza wamiliki wa misitu ya Jamii ikiwemo ya vijiji kuisimamia kikamilifu kulingana na Sheria, Kanuni na Miongozo iliyopo akisisitiza kuwa iwapo mpangokazi aliouzindua utatekelezwa ipasavyo, utawezesha uhifadhi na matumizi endelevu misitu ya jamii na pia kuchangia maendeleo endelevu katika sekta nyingine.
”Ili nyaraka hizi zieleweke vyema na kutumika kwa ukamilifu miongoni mwa wadau walio wengi, ninaiagiza Idara ya Misitu na Nyuki izifanyie tafsiri nyaraka hizi ziwe kwa lugha ya kiswahili na zisambazwe kwa wadau wengi kwa kadri itakavyowezekana”.Aliongeza Balozi Dkt Chana





No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇