LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

May 14, 2022

SHAKA APOKELEWA KWA KISHINDO MKOANI MANYARA

 


Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Taifa   Shaka Hamdu Shaka, ambaye ni mlezi wa CCM mkoa wa Manyara   akisalimiana na Mkuu wa Mkoa Wa Manyara Mhe Makongoro Nyerere alipowasili mkoani Manyara kwa ziara ya siku mbili kukagua uhai wa chama.

Katibu  wa Itikadi na Uenezi CCM Taifa  Shaka Hamdu Shaka, Akipewa Rungu na Laiguanani Mkuu wa Jamii ya Watu wa Simanjiro ikiwa ni Ishara ya Kumsimika kuwa kiongozi wa Ngazi ya Juu katika jamii hiyo na Kumpa Jina La “OLE SHAKA”

 

Katibu  wa Itikadi na Uenezi  CCM Taifa  Shaka Hamdu Shaka, akiwa Amembeba Mwanafunzi wa Shule ya Msingi ya Magugu kitengo Cha Watoto Wenye Ulemavu Azmina Swedy mara baada ya kumkabidhi kadi ya Bima ya Afya iliyotolewa msaada na Uongozi wa CCM Mkoa wa Manyara.

  

Katibu  wa Itikadi na Uenezi  CCM Taifa  Shaka Hamdu Shaka, akizungumza katika Mkutano wa Ndani wa Viongozi na Wanachama wa CCM Katika Wilaya za Babati Mjini Na Vijijini katika Ziara yake ya Kukagua Uhai Wa Chama Mkoan humo.

Katibu  wa Itikadi na Uenezi CCM Taifa  Shaka Hamdu Shaka, Akizungumza na Kamati ya Siasa Mkoa wa Manyara pamoja na Wilaya zake katika Ukumbi wa Vikao Ofisi za CCM Mkoa wa Manyara 

Viongozi na Wanachama wa CCM wakicheza pamoja Ngoma ya Kikundi Cha Msanja Mkoani Manyara

 

Wanachama Mbalimbali wakinyanyua Vipeperushu Juu wakati wa Mkutano wa Ndani wa Katibu CCM wa Itikadi na Uenezi Taifa  Shaka Hamdu Shaka,pamoja na Viongozi na Wanachama wa Mkoa wa Manyara 

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages