LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Nov 19, 2021

MATUKIO KATIKA PICHA KATIBU MKUU CCM AKIWA ZIARA WILAYANI KASULU

 


Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Daniel Chongolo akiteta jambo na Mwenyekiti wa Shina namba 1 lililopo mtaa wa Sunzu Juma Rugina (katikati) pamoja na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kasulu  Ndugu Mbelwa Chidebwe (kulia) wakati wa mkutano na wakazi wa shina hilo Kasulu mkoani Kigoma. (Picha na CCM Makao Makuu) 

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Daniel Chongolo akihutubia wakazi wa Shina namba 1 lililopo mtaa wa Sunzu Kasulu mkoani Kigoma ikiwa sehemu ya ziara yake ya kukagua uhai wa chama na kusimamia utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025. (Picha na CCM Makao Makuu) 

 Sehemu ya Viongozi na wakazi wa shina namba 1lililopo mtaa wa Sunzu, kata ya Kumnyika wakimsikiliza Katibu Muu wa CCM Ndugu Daniel Chongolo ambaye yupo mkoani Kigoma kwa ziara ya kuimarisha uhai wa Chama na kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2020-2025. (Picha na CCM Makao Makuu) 

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Daniel Chongolo (katikati) akishiriki ujenzi wa Shule ya Sekondari Mayonga pamoja na viongozi wengine ikiwa sehemu ya ziara ya kukagua, kuhamasisha na kusimamia ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025. (Picha na CCM Makao Makuu)

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages