Tegeta, Dar es Salaam
Baba Halisi wa Kanisa Halisi la Mungu Baba amewakaribisha Wafanya Biashara ndogondogo 'Machinga', katika Ibada Maalum ya kuwabariki Wafanyabiashara hao, ambayo itafanyika Jumapili hii, Novemba 7, 2021 (Lango la Moyo Mmoja, 19 Eluli 9), Makao Makuu ya Kanisa hilo, Tegeta jijini Dar es Salaam.
"Wote Mnakaribishwa bila kujali Dini au Dhehebu maana Chanzo Halisi amekuja kuwabariki wote ( Efeso 4:6) amesema Baba Halisi katika Tangazo la mwaliko wa Machinga kuwaalika wafike kwa wingi kwenye Ibada hiyo.
Ibada hiyo ya Kuwabariki machinga, itakuwa ya nne ya kijamii kufanywa na Kanisa hilo, ikiwa imetanguliwa na Ibada ya Kuwabariki Waandishi wa Habari, Ibada ya 'Kufuta ajali' kwa waendesha bodaboda na Ibada ya kuwabariki Mama na Baba Lishe kwa ajili ya kuleta 'jiko jipya', iliyofanyika Jumapili iliyopita.
Your Ad Spot
Nov 4, 2021
Home
featured
KIJAMII
KANISA HALISI LAWAALIKA MACHINGA KATIKA IBADA MAALUM YA KUWABARIKI, ITAKAYOFANYIKA JUMAPILI HII, TEGETA JIJINI DAR ES SALAAM
KANISA HALISI LAWAALIKA MACHINGA KATIKA IBADA MAALUM YA KUWABARIKI, ITAKAYOFANYIKA JUMAPILI HII, TEGETA JIJINI DAR ES SALAAM
Tags
featured#
KIJAMII#
Share This
About Bashir Nkoromo
KIJAMII
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇