LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 31, 2021

FOUNTAIN GATE YAFUNIKA SHULE KONGWE MATOKEO DARASA LA SABA

........Yashika nafasi ya kwanza Mkoa wa Dodoma


  Mkuu wa taaluma wa shule ya Fountain Gate Academy Ayoub Martin akifurahia na wanafunzi wa shule hiyo ilipotangazwa kuwa ya nne kwa Mkoa wa Dar es Salaam na shule yao ya Dodoma kuongoza Mkoa huo kwenye matokeo ya darasa la saba.


Mkuu wa shule hiyo, Karama Khalid akifurahia na wanafunzi wa shule hiyo ilipotangazwa kuwa ya nne kwa Mkoa wa Dar es Salaam na shule yao ya Dodoma kuongoza Mkoa huo kwenye matokeo ya darasa la saba.



 Wanafunzi wa shule ya Fountain Gate Academy ya Tabata jijini Dar es Salaam wakishangilia baada ya shule yao kuziangusha baadhi ya shule kongwe kwenye matokeo ya darasa la saba yaliyotangazwa hivi karibuni kwa shule hiyo kuwa ya nne Mkoa wa Dar es Salaam wakati ile ya Dodoma ikiongoza mkoa huo.




Na Mwandishi Wetu

SHULE  za Fountain Gate Academy zimeendelea kufanya vizuri ambapo kwenye matokeo ya darasa la saba mwaka huu zimefanikiwa kufanya vizuri zaidi na kuzipita baadhi ya shule kongwe nchini kiwilaya, Mkoa na kitaifa.

Kwenye matokeo hayo yaliyotangazwa na NECTA mwishoni mwa wiki, shule ya Fountain Gate Dodoma imekuwa ya kwanza kati ya shule 552 za Mkoa huo, ya kwanza pia kwenye halmashauri yake kati ya shule 104 na ya 171 kitaifa kati ya shule 11,909 .

Kwenye matokeo hayo kwa upande wa Fountain Gate  Tabata imefanikiwa kuwa ya nne kati ya shule 92 za Wilaya ya Ilala na imekuwa ya 25 kati ya shule 498 Mkoa wa Dar es Salaam wakati kitaifa imekuwa ya 111 kati ya shule 11,909.

Mkurugenzi wa shule hizo, Japhet Makau alisema kwa upande wa shule hiyo Tabata wanafunzi 141 ndio walifanya mtihani huo na kati yao, 114 wamepata wastani wa alama A na 27 wamepata wastani wa alama B na hakuna C wala alama D.

Makau alisema hayo  ni mafanikio makubwa kwa shule yake kwani imefanikiwa kuzipita shule kongwe ambazo zilikuwa zikishika nafasi ya kwanza na aliwapongeza walimu kwa namna wanavyojituma kufundisha mpaka kupatikana kwa matokeo mazuri kama hayo.

Makau alisema haikuwa kazi rahisi kupata matokeo mazuri kiasi cha kuzipita shule kongwe hivyo walimu wa shule hizo wanastahili pongezi kwani wamekuwa wakifanyakazi usiku na mchana kuhakikisha wanafunzi hao wanaandaliwa vizuri kwaajili ya mitihani ya kitaifa.

“Nawashukuru wazazi kwa kuendelea kutuamini na kutupa watoto wao tuwaleee na kwa mafanikio haya napenda kuwaahidi kwamba hatutabweteka tutaendelea kufundisha kwa bidii kuhakikisha shule zetu zinaendelea kuwa juu kitaaluma na hata siku moja kushika nafasi ya kwanza kitaifa,” alisema Makau.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages