LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 15, 2021

MBUNGE JANETH MAHAWANGA AZINDUA VIKUNDI 16 VYA WAJASIRIAMALI KATA YA GOBA

Goba, Dar es Salaam
Mbunge wa Viti Maalumu kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) anayewakilisha Mkoa wa Dar es Salaam, Janeth Mahawanga amezindua  vikundi 16  vya wanawake wajasiriamali  katika Kata ya Goba, Wilayani Ubungo.

Vikundi hivyo viko chini ya  mwavuli wa Goba Women Coporate, vilizinduliwa katika  sherehe za  Siku ya Wanawake Goba.

Akizungumza  wakati wa uzinduzi huo leo Mbunge Janeth , amesema  uanzishwaji wa vikundi ni utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na mwito wa Mwenyekiti wa Chama, Rais  Samia Suluhu Hassan.
 
Aliwataka wanake mkoani Dar es Salaam kutumia fursa zilizopo mkoani humo ili kujikwamua kiuchumi.


“Wanawake wa Dar es Salaam ile hali tu ya kuishi hapa   Dar ni fursa ya kutosha, kwa sababu tumezungukwa na fursa nyingi ambazo ni rahisi kuzifikia,”amesema  Mbunge  Mahawanga.

Ameeleza, kiu yake  kama mwakilishi wa wanawake Bungeni ni kuona Dar es Salaam, inakuwa ya kwanza  kupata matokeo bora katika vikundi.

“Nitumeni  niwatumikie.Niiteni na nitakuja tuongee namna ya kujikwamua kiuchumi. Fedha  za mikopo isiyo na riba zipo  nyingi katika halmshauri zetu, hivyo suala la mitaji siyo changamoto kabisa,”ameeleza Janeth Mahawanga.

Amefafanua pia Rais Samia, ameeleza kuwa Ikulu kuna fedha  zinazoweza  kukopeshwa kwa njia ya vikundi hivyo ni lazima wanawake kujiunga katika vikundi hivi.

“Tuwaone wataalamu wa maandiko, watuandikie  miradi. Tusajili vikundi . Wanawake hatuwezi kupata mafanikio kama  ni wavuvi,  hatuwezi kujifunza,  kutafuta watalaamu  na kuwa wazito wa kukopa,”amebainisha  Mbunge huyo.

Amehimiza  vikundi vya wajasiriamali vya wanawake alivyo zindua na vingine mkoani  humo, kudumisha upendo  na kuacha kutengeneza matabaka  ya walionacho na wasio nacho au wakongwe na wapya.

“Hii inauwa  vikundi. Wote jioneni mko sawa. Fuateni katiba ya kikundi. Tupande mbegu mpya  ya upendo,”amesema.

Awali  mlezi wa Goba Women Coporate,  Imgard  Mchopa, ameeleza ,  walianzisha umoja huo miaka saba iliyopita.

“Wazo lilianza mwaka 2014, kutokana na Goba kutishiwa na uhalifu. Wanawake tuliamua kutambuana kwa kujiunga katika kundi moja. Hapo vikazaliwa sasa vikundi vya ujasiriamali,”amesema.

Ameongeza kuwa  hadi sasa wana wanachama zaid ya 800 na wamekuwa wakijishughulisha na shughuli mbalimbali za ujasiriamali na wana malengo ya kuanzisha miradi mbalimbali ikiwemo kuchukua tenda za usafi na  ulinzi.

“Hata hivyo  tunaomba kuwezshwa kupata mikopo ya halmashauri ili tupate mitaji. Kupata elimu ya ujasiriamal na vikundi,”amebainisha.

Mbunge wa Viti Maalum, Janeth Mahawanga (kulia) na Mlezi wa Umoja wa Wanawake wa Kata ya Goba, Imrgard Mchopa wakionyesha Katiba ya Umoja huo, baada ya kuizindua, Dar es Salaam, leo.

Mbunge wa Viti Maalum, Janeth Mahawanga akizungumza wakati wa uzinduzi huo.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages