LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 18, 2021

MAJAJI WALIA NA CHANGAMOTO YA UCHACHE WA MAWAKILI WA SERIKALI NCHINI

Na Mwandishi  Maalum, Kagera
Imelezwa kuwa idadi ndogo ya Mawakili wa Serikali, wakiwamo Waendesha Mashtaka katika baadhi ya Mahakama Kuu za Kanda, ni moja ya changamoto zinazo kwamisha utekelezaji wa utoaji hakijinai

Changamoto hiyo imebainika wakati wa ziara ya kikazi ya Makatibu Wakuu watatu wakiongozwa na  Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Profesa Sifuni Mchome katika Mikoa ya Tabora, Kigoma na Kagera.

Jaji Athumani Matuma Kirati wa Mahakama Kuu Kigoma, aliwaeleza Makatibu Wakuu hao kwamba,   ukamilishaji wa  idadi ya kesi ambazo wamejipangia unaathiriwa sana na uchache wa Waendesha Mashtaka na Mawakili wa Serikali.

“Sisi katika Mahakama Kuu Kigoma, tumejipangia utararibu wetu wa ndani wa kumalisha kesi tulizo nazo kwa muda, na  tunakwenda vizuri sana kuanzia  hapa Mahakama Kuu mpaka  mahakama za chini.

Lakini  tunashikwa mashati na wadau wetu  wakiwamo waendesha  mashtaka  ambao ni wachache, tunaomba  msitushike mashati ili tufikie malengo yetu tuliyojiwekea” akasema Jaji Athumani  Kirati.

Jaji  Kirati anakwenda mbali  kwa kueleza kwamba, katika  Jengo lao  jipya wametenga Ofisi kwaajili ya Mawakili  hao wa Serikali,  lakini  Ofisi  zimekuwa  tupu kwa kuwa hakuna  mawakili wa serikali na kama wapo basi ni moja, jambo analosema linakwamisha  si tu katika uendeshaji wa mashataka bali hata pale unapotakiwa  ushauri wa kisheria.

Uchache  wa Waendesha Mashtaka katika Mkoa wa Kigoma, pia ulichagiwa na Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Kanali Isack Mwakisu ambaye alisema Mahakama ya Hakimu Mfawidhi Kasulu ina mahakimu watatu lakini waendesha mashtaka  wawili na hivyo  Hakimu mmoja anashindwa kufanya kazi  ipasavyo.

“ Tutafurahi sana kupata  mawakili wa serikali wa kutosha, na wilaya yangu ipo tayari kuaanda mazingira mazuri ya ufanyaji kazi” akabainisha Kanali Mwakisu,

Naye Dkt Ntemi Kilekamajenga, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba,  anasema  Kanda  hiyo ina waendesha mashataka na mawakili wa serikali wachache hali inayokwamisha  utekelezi wa majukumu yao.

Anasema kwa mfano kitakapo anza kikao  maalumu ya kusikiliza kesi mapema mwezi ujao, baadhi ya  Mahakama zitashindwa kuendesha kesi kwa kukosa mawakili wa serikali kwani wachache waliopo watakuwa katika vikao hivyo maalum.

“ Tunaiomba serikali iajiri mawakili wa seriali wa kutosha ili tusikwame, hawa ni  watu muhimu hatuwezi kuendesha kesi bila wao, na tutakapoanza vikao maalum hapana shana  mahakimu wengine hawataweza kuendelea na kesi zao, tunaomba tusaidiwe katika hili.

Kwa upande wa Mahakama Kuu Kanda ya Tabora, kuna  waendesha mashtaka wanane ikilinganishwa na idadi ya mahakimu na mwanasheria mmoja wa Serikali, hali ambayo  nayo imetajwa kuchelesha utoaji wa haki.

Mikoa ya Tabora, Kigoma na Kagera ni mikoa ambayo inamuingiliano mkubwa wa watu kutoka nchi za jirani, lakini pia ina idadi kubwa ya kesi za jinai zikiwamo za  mauaji, migogoro ya ardhi, ubakaji, na wahamiaji haramu  kutoka nchi jirani.

Akijibu hoja hiyo ya uhaba wa  mawakili wa serikali, Katibu Mkuu Sifuni Mchome, amesema Wizara imeomba kibali cha kuajiri mawakili wa serikali na wanasubiri jibu.

Aidha pamoja na changamoto mbalimbali zikiwamo za uendeshaji wa mashauri kwa kupitia mfumo wa  TEHAMA, mfumo ambao ulielezwa na Majaji hao  kwamba bado unachangamoto kadhaa zikiwamo za    magereza kukosa vifaa vya  TEHAMA na  uhafifu wa mtandao,, Katibu Mkuu amezipongeza Mahakama  katika  mikoa hiyo kwa utekelezaji mzuri wa umalizaji wa kesi.

Vilevile amesifu ushirikiano baina ya Taasisi ambazo zinahusika na mnyororo wa utoaji haki,huku akisisitiza  kwamba, ushirikiano uendelezwe pasipo kuingiliana  katika utekelezaji kazi wa kila Taasisi,

Jaji Athumani Matuma Kirati akizungumzia hali ya utoaji haki Katika Mahakama Kuu Kanda ya Kigoma, kwa Makatibu Wakuu Sifuni Mchome, John Jingu na Christopher Kadio. Pamoja na  mambo mengine,  Jaji Kirati alielezea uhaba wa mawakili wa serikali na waendesha mashtaka unavyowakwamisha katika utekelezaji wa  majukumu yao  ya utoaji wa haki kwa wakati. Makatibu  Wakuu hao walikuwa katika ziara ya kikazi  katika mikoa ya Tabora, Kigoma na Kagera. (Na Mpigapicha Maalum)

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages