LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 31, 2021

KATIBU MKUU UWT DK. NYIMBI AZINDUA KWA KISHINDO JOGGING YA UWT MKOA WA DAR , ASEMA MAZOEZI NI ZAIDI YA 'PANADOL'

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Umoja wa wanawake Tanzania (UWT) Dk. Phils Nyambi (Wapili kushoto) akipiga hatua za kikakamavu, wakati akiongoza Jogging ya UWT mkoa wa Dar es Salaam, leo ambayo ilianzia Viwanja vya Karimjee na kumalizikia Viwanja vya Mnazi Mmoja ambako alizidua rasmi Jogging ambayo itakuwa ikifanywa na UWT mkoa wa Dar es Salaam kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi. Hata hivyo wakati wa uzinduzi huo Dk, Nyimbi alioutaka aliuagiza Uongozi wa UWT mkoa huo kuandaa Jogging kila Jumamosi katika kila Wilaya za mkoa huo. Kushoto ni Mjumbe wa Baraza Kuu la UWT Taifa na Mjumbe wa NEC Angel Akilimali akifuatiwa na Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Dar es Salaam Florence Masunga, Kulia ni Katibu wa UWT mkoa huo Grace Haule,
Mwalimu wa Mazoezi, akiendesha mazoezi ya kuchangamsha mwili kwa washiriki kabla ya kuanza matembezi na mchakamchaka barabarani.
Katibu Mkuu wa UWT Dk. Phils Nyimbi akionekana kujituma pamoja na Wana Jogging wenzake wakati wa mazoezi hayo ya kuchangamsha mwili, katika Viwanja vya Karimjee.
Mbunge wa Jimbo la Temeke Dorothy Kilave (kushoto) naye alikuwepo katika Jogging hiyo. Wapili kutoka kwa Mbunge huyo ni Mwenyekiti wa UWT Dar es Salaam Florence Kilave akionekana kujituma.
Polisi wa Usalama Barabarani akiwaelekeza Barabara au mitaa watakayopitia wakati wa mchakamchaka na matembezi ya Jogging walipokuwa wanajiandaa kutoka kwenye Viwanja vya Karimjee kwenda hadi Mnazi Mmoja.
Safari ikiwa imeanza huku ikiongozwa kwa ukakamavu na Katibu Mkuu wa UWT Dk. Phils Nyimbi.
Matembezi na mchakamchaka vikiendelea
 
Msafara ukiwa umeingia Barabara ya Bibi Titi Mohammed ambaye ndiye Muasisi wa UWT.
Msafara ukiendelea hapa aliyepo mbele kabisa ni Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Njombe Scholastika Christian Kevela.
Msafara ukiendelea, na hapa aliyewatangulia wenzake ni Mjumbe wa NEC Angel Akilimali.
Msafara ukikatiza eneo la Kisutu kwenda Mnazi mmoja. hapa aliyeko Mbele ni Katibu Mkuu wa UWT Dk. Phils Nyimbi.
Msafara ukiingia katika Viwanja vya Mnazi Mmoja

Katibu Mkuu wa UWT Dk. Phils Nyimbi akiwaongoza viongozi wa Jumuiya hiyo mkoa wa Dar es Salaam kuingia Viwanja vya Mnazi Mmoja.

 

Baada ya Kuwasili Mnazi mmoja hekaheka zikaendelea

👇

Katibu Mkuu wa UWT Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Dar es Salaam wakijimwayamwaya na mwana Jogging mwenzao.
Katibu Mkuu Dk. Phils Nyimbi wakiimba nyimbo huku wakiwa mbele ya bango lenya Picha ya Mwenyekiti wa CCM Rais Samia Suluhu Hassan ambalo walitoka nalo Mnazi Mmoja.
Wakiendelea kujimwaya mwaya kwa furaha.
Katibu Mkuu wa UWT Dk. Phils Nyimbi na viongozi wa Meza Kuu wakiwa wamesimama kushangilia jambo, wakati shamrashamra za Jogging hiyo kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Katibu wa UWT mkoa wa Dar es Salaam Grace Haule (kushoto), akizungumza na kutoa utambulisho wa viongozi waliohudhuria uzinduzi wa Jogging hiyo, kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja.
Mbunge wa Jimbo la Temeke Dorothy Kilave akizungumza baada ya kutambulishwa na Grace Haule na kupewa nafasi ya kusalimia Wana Jogging waliohudhuria.

Mjumbe wa Baraza Kuu la UWT Taifa na Mjumbe wa NEC Anjel Akilimali akizungumza baada ya kutambulishwa na Grace Haule kuwasalimia na kuzungumza machache na Wana Jogging waliohudhuria. Akilimali pia ni Mtumishi wa Vyombo vya Habari vya Chama Cha Mapinduzi (CCM) vya Uhuru Media Group.

Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Dar es Salaam
Florence Masunga akizungumza baada ya kuinuliwa na Grace Haule kusalimia na kuzungumza kisha kumkaribisha mgeni rasmi Dk. Phils Nyimbi kuhutubia na kuzindua Jogging hiyo kwa UWT mkoa huo. "Ndugu Katibu Mkuu wetu karibu uzungumze na kutuzinduliwa Jogging yetu", akasema Mama Masunga.
Katibu Mkuu wa UWT Dk. Phils Nyimbi akizungumza na Wana Jogging baada ya kukakaribishwa kwa heshima kubwa na Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Dar Mama Florence Masunga, kuzungumza na kuzindua Jogging hiyo kwa UWT mkoa wa Dar es Salaam.

"Tanzania na hususan Wanawake wenzangu tusitegemee 'Panadol' kujenga mwili, bali tufanye mazoezi ndiyo yanayojenga mwili kwa  kutukinga na magonjwa yasiyoambukizwa, Hata ukipatwa na Uviko kama unafanya mazoezi makali yake yanakuwa madogo...." akasema Dk. Phils Nyimbi huku viongozi meza kuu na Wana Jogging waote wakimsikiliza kwa makini na wengine wakimshangilia.
Baadhi ya Wana Jongging wakimshangilia Dk. Nyimbi baada ya kutamka kuzindua Jogging hiyo.
Baadhi ya Wana Jongging wakiendelea kumshangilia Dk. Nyimbi baada ya kutamka kuzindua Jogging hiyo.

Baadhi ya Wana Jogging wakiwa makini kumsikiliza Dk. Nyimbi.

Kisha Dk. Nyimbi akasuka jukwaani kuselebuka na Wana Jogging baada ya kuzindua rasmi Jogging hiyo kwa  UWT mkoa wa Dar es Salaam👇

Pamoja na kuselebuka, Dk. Nyinmbi (kushoto), akaamua kumtuza 'minoti' Mwana Jogging mmoja ambaye alionyesha kucheza muda wote bila kupumzika licha ya kushiriki kutembea na kufanya mchakamchaka kutoka Karimjee hadi Mnazi Mmoja.
Dk. Nyimbi akaamua kumbandika noti mwana Jogging huyo, huku Mbunge wa Temeke Dorothy Kilave (kulia) naye akitazama kwa hamasa.
Dk. Nyimbi akambandika noti Mwana Jogging mweinge ambaye naye alionyesha hamasa ya kutosha wakati wakiselebuka.
Mbunge wa Temeke Mama Kilave akaamua kumuunga Mkono Katibu Mkuu Dk. Nyimbi, kuwatuza  Wana Jogging hao waliotia fora.

"Chukua hii.." akasema Mama Kilave akimbandika noti mwana Jogging huyo.
Mambo yakawa motooo....

Kuselebuka kukiendelea.. Hapo ni Mwana Jogging Diwani Mama Mtemvu akiselebuka na Mwana Jogging mwenzake.

Kisha ukafika wakati wa Katibu Mkuu Dk. Nyimbi kukabidhi kadi za UWT kwa Wanachama wapya Wadada.👇

👇
👇

👇
Katika kutoa kadi hizo kwa wanachama wadada, Dk. Nyimbi alikabidhi kadi kumi ambao walipokea kwa niaba ya wengine. Kwa Mujibu wa Katibu wa UWT mkoa wa Dar es Salaam Grace Haule Wanachama hao wapya waliostahili kupata kadi walikuwa 50.

Wanachama wapya Wadada wa UWT wakionyesha kadi zao baada ya kukabidhiwa
 
Kisha makundi mbalimbali yakapigwa picha na viongozi za kumbukumbu👇

👇
👇
---------
"Mkuu umeionaje shughuli yetu", inaelekea ndivyo Katibu wa UWT mkoa wa Dar es Salaam ndivyo alivyokuwa akimuuliza Boss wake Katibu Mkuu wa UWT Dk. Nyimbi mwishoni mwa hafla hiyo. Kushoto ni M-NEC Angel Akilmali.


 
Photo Album, Karimjee👇

























Ends. 
©2021 CCM Blog/Bashir Nkoromo

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages