Mbunge
wa viti maalum wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Santiel Kirumba (wa pili
kushoto) akikabidhi Kompyuta kwa ajili ya shule ya Sekondari ya
Wasichana Kishapu ‘Kishapu Girls’ mkoani Shinyanga ili kuwajengea uwezo
wa TEHAMA wanafunzi hao. Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe.
Joseph Modest Mkude.
Na Kadama Malunde
Mbunge
wa viti maalum wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Santiel Kirumba amekabidhi
vifaa vya TEHAMA zikiwemo Kompyuta 5 , Printa 1 pamoja na spika zake
vyenye thamani ya milioni 15 kwa ajili ya shule ya Sekondari ya
Wasichana Kishapu ‘Kishapu Girls’ mkoani Shinyanga zisaidie kuwajengea uwezo wa TEHAMA wanafunzi hao.
Akikabidhi
vifaa hivyo Jana Jumamosi Agosti 14,2021 Mhe. Kirumba amesema kuwa
kompyuta hizo zitaenda kuwajengea uwezo wa TEHAMA wanafunzi na kuongeza
ufaulu wa shule hizo.
Alisema
Kompyuta hizo ni sehemu ya Computer 30 alizoomba kwa kushirikiana na
Wabunge wenzake wa Mkoa wa Shinyanga na kutolewa na Serikali kupitia
Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF).
Mhe.
Kirumba aliishukuru na kuipongeza Serikali ya awamu ya sita kupitia
Wizara hiyo na taasisi yake ya UCSAF kwa kuthamini na kuisimamia vema
ilani ya uchaguzi ambayo imezungumzia kuongeza matumizi ya TEHAMA na wao
wanatekeleza kwa vitendo huku akizitaka shule zilizonufaika na vifaa
hivyo kuvitunza na kuvitumia kuleta matokeo tarajiwa kwa walimu na
wanafunzi wa shule hizo.
Mkuu
wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude alisema vifaa hivyo vya
TEHAMA vitasaidia kuchochea ukuaji wa matumizi ya TEHAMA na kuwaandaa
vijana na mabadiliko ya teknolojia duniani.
Mapema
Jana Agosti 14,2021 Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
Mhe. Mhandisi Kundo Mathew alikabidhi vifaa vya TEHAMA kwa ajili ya
shule 6 za Sekondari zilizopo ndani ya Mkoa wa Shinyanga ikiwemo shule
hiyo ya Kishapu Girls vyenye thamani ya shilingi Milioni 50
vilivyotolewa na Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF).
Makabidhiano
hayo yalifanyika Mkoani Shinyanga kati ya Naibu Waziri huyo na Mbunge
wa viti maalum wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Santiel Kirumba, Mkuu wa Wilaya
ya Shinyanga Mhe. Janista Mboneko, na Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya
Shinyanga Nice Munisi ambapo jumla ya kompyuta 30 na printa 4
zilikabidhiwa rasmi.
Akizungumza
mara baada ya makabidhiano hayo Mhandisi Kundo alisema kuwa Serikali
kupitia UCSAF imeendelea kutekeleza mradi wa kupeleka vifaa vya TEHAMA
katika shule za umma ili kuchochea ukuaji wa matumizi ya TEHAMA na
kuwaandaa vijana na mabadiliko ya teknolojia duniani.
Pia
alizungumzia mradi wa wasichana na TEHAMA unaotekelezwa na UCSAF ambao
unalenga kuwawezesha na kuwajengea uwezo watoto wa kike katika TEHAMA
ndio maana katika upelekaji wa vifaa vya TEHAMA katika shule za
sekondari Mfuko huo unaangazia na Shule za Sekondari za wasichana.
“Wizara
kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote tuna kipengele kingine cha
kuwawezesha watoto wa kike na TEHAMA ili kuwajengea uwezo na hatimaye
kutengeneza wataalam wa TEHAMA wengi zaidi nchini kwa sababu mpaka sasa
wataalam wa TEHAMA wanawake ni wachache kuliko wa kiume lengo letu ni
kwamba tunapoongelea 50 kwa 50 ionekane kwa vitendo”, alisema Mhandisi Kundo.
Kwa
Upande wa Mkuu wa Uendeshaji wa UCSAF Mhandisi Albert Richard alisema
kuwa vifaa hivyo vya TEHAMA vilivyokabidhiwa katika Mkoa wa Shinyanga ni
miongoni mwa jumla ya kompyuta 800 na printa 20 zinazoendelea
kusambazwa katika ya shule za sekondari za umma ambazo zilianishwa
katika bajeti ya mwaka wa fedha 2020/22.
Mbunge
wa viti maalum wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Santiel Kirumba (wa pili
kushoto) akikabidhi Kompyuta kwa ajili ya shule ya Sekondari ya
Wasichana Kishapu ‘Kishapu Girls’ mkoani Shinyanga ili kuwajengea uwezo
wa TEHAMA wanafunzi hao. Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe.
Joseph Modest Mkude
Mbunge
wa viti maalum wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Santiel Kirumba (wa pili
kushoto) akikabidhi Kompyuta kwa ajili ya sshule ya Sekondari ya
Wasichana Kishapu ‘Kishapu Girls’ mkoani Shinyanga.
Mbunge
wa viti maalum wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Santiel Kirumba (wa pili
kushoto) akikabidhi Printer kwa ajili ya shule ya Sekondari ya Wasichana
Kishapu ‘Kishapu Girls’ mkoani Shinyanga
Mbunge
wa viti maalum wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Santiel Kirumba (wa pili
kushoto) akikabidhi Printer kwa ajili ya shule ya Sekondari ya Wasichana
Kishapu ‘Kishapu Girls’ mkoani Shinyanga
Zoezi la makabidhiano ya vifaa vya TEHAMA likiendelea katika shule ya sekondari ya Wasichana Kishapu.
Zoezi la makabidhiano ya vifaa vya TEHAMA likiendelea katika shule ya sekondari ya Wasichana Kishapu.
Zoezi la makabidhiano ya vifaa vya TEHAMA likiendelea katika shule ya sekondari ya Wasichana Kishapu.
Wanafunzi wakifuatilia Zoezi la makabidhiano ya vifaa vya TEHAMA katika shule ya sekondari ya Wasichana Kishapu.
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇