LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jun 25, 2021

SERIKALI YA CCM KUTOA KIPAUMBELE KATIKA SEKTA YA ELIMU

Dodoma, jana.

Akizungumza Alhamisi 24 Juni 2021 kupitia jukwaa la walimu waliofanya ziara ya kimafunzo makao makuu ya CCM Dodoma, Katibu Halmashauri Kuu ya Taifa Itikadi na Uenezi, Ndg. Shaka Hamdu Shaka, amesema Serikali ya CCM inatambua na kuthamini mchango mkubwa unatolewa na  walimu nchini katika  kuelimisha, kuwaandaa  na kulea vyema vijana hivyo kipaumbele cha serikali ya awamu ya sita ni kuhakikisha sekta hiyo inamarika.


"Mhe Rais Samia  baada wanafunzi 11,000 kukosa mikopo elimu ya juu, ameongeza billioni 70 ili kuwanufaisha walikosa waendelee mikopo na  ameongeza bujeti ya billioni 300 kwa bodi ya mikopo ili waweza kutoa huduma kwa wanafunzi wengi zaidi. Chama kitafutilia kwa karibu ili kuona ufanisi wake katika kuondoa vilio na malalamiko kwa wanafunzi." Alisema  Shaka.


Amefahamisha kuwa  serikali ya CCM  imeendelea kutekeleza ilani uchaguzi  2020/2025 kwa  kuboresha mazingira ya watumishi nchini ikiwemo walimu ambapo  serikali imepunguza kodi “payee” kutoka asilimia 9 ya awali hadi asilimia 8, Lakini pia serikali ya CCM imetoa ajira kwa walimu 6000 na  imeelekeza watumishi wote wenye sifa wakiwemo walimu wapandishwe madaraja na kulipwa malimbikizo yao yote jambo ambalo uratibu wake unaendelea. 


Aidha Katibu Mwenezi ametoa Rai kwa walimu nchini  kutoa elimu juu ya matumizi mazuri ya mitandao ya kijamii kwa vijana, sambamba na  kuendelea kuwajengea uzalendo na kutambua thamani ya utaifa wao.


Viongozi wa Jukwa la walimu wako katika mafunzo ya Siku mbili mkoani Dodoma ambapo pia wamepata fursa ya kutembelea maeneo mbali mbali kujifunza shuhuli za uendeshaji wa taasisi husika.

Picha mbalimbali kuhusu tukio hilo👇










Imeandaliwa na Idara ya Itikadi na Uenezi CCM HQ

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages