LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Apr 19, 2021

SERIKALI YAMSIMAMISHA KAZI KURUGENZI MABASI YA MWENDOKASI (UDART)


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi Mkurugenzi wa Fedha na Maendeleo ya Biashara wa Wakala wa Mabasi yaendayo haraka nchini (UDART) Suzana Chaula,  huku akiweka wazi kuwa tatizo lililopo kwenye mradi huo  si uwezo bali ni usimamzi mbovu.


Waziri Mkuu Majaliwa amefikia uamuzi huo hii leo wakati wa ziara yake katika baadhi ya vituo vya mabasi yaendayo haraka mkoani Dar es salaam, ambapo pia  amebaini utendaji kazi na ufuatiliaji mbovu katika mradi huo.

“Tunataka tujenge mradi awamu ya tatu kwenda Gongo la Mboto, na tunajenga awamu hii kwa  kukusanya fedha kununua mabasi kwa ajili ya awamu nyingine uwezo huo upo,  hatuwezi kuvumilia msimamizi ambaye hawezi akiwemo Mkurugenzi wa fedha, Hii fedha sisi tumekopa World Bank na tunalipa fedha yetu ya ndani ya walipa kodi wa Tanzania, leo tunaweka watu hawafanyi kazi vizuri,”amesema Waziri Mkuu.

Amesema mfumo unaotumika wa uuzaji wa tiketi ni mbovu, na unaikosesha Serikali mapato mengi jambo.ambalo halikubaliki.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages