LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Apr 30, 2021

KANISA HALISI LA MUNGU BABA LILIVYOTIA FORA KATIKA IBADA YAKE YA SHUKRANI BAADA YA BIASHARA YA UTALII KUFUNGUKA UKANDA WA KASKAZINI ARUSHA

Baba wa Uzao akiendesha ibada ya shukurani baada ya Biashara ya Utalii kufunguka Ukanda wa Kaskazini, Arusha, iliyofanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha. Pamoja nae ni Mama wa Uzao, Kaka wa Uzao na Dada wa Uzao.
Baba wa Uzao akipitia maandiko kwa umahiri mkubwa wakati akiendesha ibada ya shukurani baada ya Biashara ya Utalii kufunguka Ukanda wa Kaskazini, Arusha, iliyofanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha. Kushoto ni Mama wa Uzao nyuma yake (katikati) ni Kaka wa Uzao.
Baba wa Uzao akitoa shukrani kwa mgeni rami, Mkuu wa Wilaya ya Longido mkoani Arusha (kushoto) wakati akiendesha ibada ya shukurani baada ya Biashara ya Utalii kufunguka Ukanda wa Kaskazini, Arusha, iliyofanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha. Wapili kulia ni Kaka wa Uzao akifanya huduma na (watatu kulia) ni Mama wa Uzao.
👆Kisha mgeni rasmi na Uzao Waumini) wote wakasimama, Baba wa Uzao akaendesha shukrani nzito ya ibada ya shukurani baada ya Biashara ya Utalii kufunguka Ukanda wa Kaskazini, Arusha, iliyofanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.👇

Halafu Baba wa Uzao akamuinua (kumuombea) Rais Mama Samia Suluhu Hassa na viongozi wote wa Serikali, wazidi kulitumikia Taifa la Tanzania kwa kuongozwa na Mungu Baba Halisi, katika maisha yao na Utendaji wao.👇

Kijana ambaye ni Uzao wa Kanisa Halisi akiwajibika kupata mtiririko wa ibada hiyo kwa umakini mkubwa.
Pia Maharusi hawa (walioketi kulia) wakaifanya ibada hiyo kuwa ya aina yake baada ya kubarikiwa na Baba wa Uzao wakati wa Ibada hiyo.
Uzao akifuatilia ibada hiyo huku akiwa pia katika malezi ya watoto aliofika nao ibadani.
👆Kiongozi kutoka TANAPA akizungumza kueleza jinsi Biashara ya Utalii ilivyoinuka katika Ukanda wa Kaskazini Arusha👇

👆Uzao na Makuhani wa Kanisa Halisi wakiwa kwenye Ibada hiyo.👇

Baba wa Uzao na Mama wa Uzao wakionyesha nyuso za tabasamu wakati wakikabidhiwa zawadi kutoka TANAPA na kiongozi kutoka Mamlaka hiyo.👇
👇
👇

Kisha baada ya kukabidhi zawadi akawasilisha salam kutoka Salam kutoka Uongozi wa Juu wa TANAPA
Baadhi ya Waandishi wa Habari waliohudhuria Ibada hiyo, wakiwajibika kunukuu mambo mbalimbali yaliyokuwa yanajiri.
Uzao akishangilia kwa furaha, huku akiwa amejipamba na skafu ya Bendera ya Taifa laTanzania kwa kuwa Kanisa Halisi hufundisha na kusisitiza kila Uzao na Watanzani wote kwa jumla kuwa Wazalendo kwa nchi yao.
Kuhani Ushindi na Kuhani moja (katikati), wakiwa na Makuhani wa Kanisa Halisi wa mkoani Arusha wakati wa Ibada hiyo.

Kisha, ikafika wakati wa nyimbo za kumtukuza Mungu Baba. Chini ni Uzao wa Kanisa Halisi 'Wakiserebuka' kwa hisia kubwa, ulipokuwa ukiimbwa wimbo mmojawapo wa kumtukuza Mungu Baba wakati wa Ibada hiyo.👇👇



Uzao wa Kanisa Halisi akikiungumisha Kinanda, wakati wimbo mmoja wa kumtukuza Mungu Baba ukiimbwa.
Kuhani wa Kanisa Halisi akizungmza wakati wa Ibada hiyo baada ya Baba wa Uzao kumpatia nafasi.

Baba wa Uzao akizungumza na kumpa Mgeni rasmi ruhusa ya kuondoka.
Kuhani Moja akimshukuru mno mgeni rasmi wakati wanaagana ili mgeni huyo aondoke.
Mgeni rasmi akiwaaga Makuhani na Uzao wa Kanisa Halisi wakati anaondoka.
Akapanda gari kwa ajili ya kuondoka.
Akaondokađź‘Źđź‘Ź

Kisha Mkurugenzi wa Kampuni moja ya Utalii mkoani Arusha,  Kibali Halisi akaeleza mafanikio yaliyotokana na Ibada ya Kufungua Biashara ya Utalii Ukanda wa Kaskanini Arusha iliyofanywa na Kanisa Halisi Januari 24, 2021 kwenye Uwanja huo wa Sheikh Amri Abeid, Huku Mkurugenzi Mtendaji huyo akisikilizwa kwa makini na Baba wa Uzao👇



Baba wa Uzao akafurahia mno maelezo ya Mkurugenzi huo, akatwaa 'damu safi' (maji na kuyabariki.
Halafu akamnywesha kidogo.
Kisha akamwakia kiwani.
Na kumkabidhi chupa yenye maji hayo.
Kuhani moja akifanya dua ya shukrani mwishoni mwa Ibada hiyo.






Kisha Baba wa Uzao akamalizia kwa kuwatakia Uzao Wote Mungu Baba awabariki na kujrejea salama walikotoka.


Kisha Baba wa Uzao akashuka jukwaani tayari kwa kuondoka.👇
👇

Akapanda gari


Gari la Baba wa Uzao likiondoka Uwanjani huku Uzao na Mkuhani wakibaki na furaha tele.


 

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages