LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Apr 6, 2021

SHIBUDA AKUMBUKA MAZURI YA HAYATI MAGUFULI, AWATAKA WATANZANIA KUCHAPA KAZI KUMUUNGA MKONO RAIS SAMIA

 Katibu Mkuu wa Baraza la Vyama vya Siasa Tanzania, John Shibuda akisaini kwenye kitabu cha maombolezo ya aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Hayati John Magufuli katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Aprili 6,2021, kabla ya kuanza kuzungumza na vyombo vya habari kuhusu hitimisho la siku 21 za maombolezo na pongezi kwa Rais wa Awamu ya Sita, Samia Suluhu Hassan.
  Shibuda akizungumza na vyombo vya habari

Wanahabari wakiwa kazini


Na Richard Mwaikenda, Dodoma

 Katibu Mkuu wa Baraza la Vyama vya Siasa Tanzania, John Shibuda amewaomba Watanzania kumuenzi aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Hayati Dkt. John Magufuli kwa mambo mazuri aliyoyafanya na kumuunga mkono kwa kuchapa kazi Rais mpya Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dodoma baada ya kusaini kitabu cha maombolezo ya Hayati Dkt Magufuli, Shibuda ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha TADEA, amempongeza Rais wa Awamu ya Sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ambapo pamoja na kumwagigia sifa lukuki amewaomba watanzania kumuunga mkono kwa kuchapa kazi ili Taifa lisonge mbele kimaendeleo.

"Rais Samia, ikubalike ujio wako ni Ari Mpya na chachu ya kuzimua kukomboana kifikra sisi kwa sisi-wewe ndiyo Darubini ya kuchanganua na kupambanua tulikotoka, tulipo na tuendako," amesema Shibuda. Ndugu, nakuomba uendelee kusikiliza clip hii ya video, Shibuda akizungumza wakati wa hitimisho la maombolezo hayo pamoja na kumpongeza Rais Samia...

IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA 
MHARIRI BLOG YA TAIFA YA CCM 
0754264203

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages