LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Mar 31, 2021

WAZIRI NDALICHAKO AKABIDHI MAGARI 38 OFISI ZA UTHIBITI UBORA WA SHULE ZA KANDA NA WILAYA NCHINI+video

  
WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako akikata utepe ikiwa ni ishara ya kukabidhi magari mapya 38   yatakayosaidia   Uthibiti Ubora wa Shule nchini katika hafla iliyofanyika Dodoma Jana. Kutoka kushoto ni Mhasibu Mkuu wa Wizara, Nicodemus Malya, 
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu,  Moshi Kabengwe na 
Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Omari  Kipanga. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA

Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Omari  Kipanga,  akizungmza wakati wa makabidhiano hayo na kuwaeleza Wathibi Ubora wa Elimu kuwa magari hayo si kwa ajili ya starehe bali kwa ajili ya kazi iliyokusudiwa.
Waziri Prof. Ndalichako akiingia kuendesha moja ya magari hayo. 
Waziri Ndalichako akiendesha gari hilo huku akiwa amempakia Naibu Waziri Kipanga.
Waziri Prof. Ndalichako akimkabidhi ufunguo wa gari Mdhibiti Mkuu wa Ubora wa Shule Kanda ya Ziwa. Victor Bwindiki.
Sehemu ya magari yaliyokabidhiwa

Sehemu ya Wathibiti Ubora wa Shule na watumishi wa wizara hiyo wakishuhudia makabidhiano hayo.








Na Richard Mwaikenda, Dodoma
 WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Pro. Joyce Ndalichako amekabidhi magari mapya 38   yatakayosaidia   Uthibiti Ubora wa Shule nchini.


Akizungumza wakati wa hafla ya ugawaji wa magari hayo jijini Dodoma leo, Prof. Ndalichako  amesema kuwa magari hayo yatagawiwa kwenye halmashauri 27 zisizo na magari, Kanda 10 na gari moja litatumika katika Ofisi ya Makao Makuu ya Wizara kwa ajili ya shughuli za ufuatiliaji.

 Amesema kuwa Wizara  kupitia Idara ya Uthibiti Ubora wa Shule ina jukumu la kusimamia mfumo wa  Uthibiti Ubora na kuifanya tathmini ya ufundishwaji katika shule na vyuo bus Ualimu na kutoka ushauri wa kitalaamu na kitaaluma wa walimu, wakufunzi na  viongozi wa Elimu ilu kuinua Ubora elimu nchini.

"Suala la usafiri ni la muhimu sana katika kuwawezesha wathibiti Ubora wa Shule na Vyuo bus Ualimu kwa wakati. Kwa kutambua hilo Serikali imeendelea kuhakikisha inawawezesha kikamilifuWathibiti hao kuifanya kuifanya kazi zao ipasavyo. Imenunua magari haya na kuendelea kuyafanyia matengenezo yaliyopo," amesema Ndalichako.

Magari hayo aina ya  Land cruiser Station Wagon ununuzi wake umegharimu zaidi ya sh. Bilioni 6. Pia magari  mengine 12 yameshanunuliwa yatawasiri nchini Mei Mwaka huu.

Ndugu, nakuomba uendelee kusikiliza kupitia clip hii ya video Waziri Prof. Ndalichako, Naibu Waziri Kipanga  wakielezea  kuhusu umuhimu wa magari hayo ...


Imeandaliwa na Richard Mwaikenda 
Mhariri Blog ya Taifa ya CCM
 0754264203

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages